Ijumaa, 3 Aprili 2026

MACHO YAKO YAFUMBULIWE

 

Ili uone kitu zaidi unachokiona au uone kile ambacho wengine hawakioni unahitaji mwanga katika macho yako.

huweze kuona kile kisichokuwa na picha/muonekano mzuri kuwa na muonekano mzuri wa kuvutia ( kisichoonekana ili kionekane ).

Vile ulivyo inategemea kiasi cha jicho lako lilivyofunguliwa kuona hivyo kadili unavyofunguliwa ndivyo unavyoona.

Ukifumbuliwa kidogo utaona kidogo na ukifumbuliwa sana utaona sana.

Kuna hatma kubwa zimefichwa katika kuona.

Ni kama watu wawili wanapoutazama mti wanapata tafsiri tofauti: mmoja anapouangalia anaweza kuona kuni nzuri zitakazo mfaa katika upishi wake na mwingine anapoangalia akaona mbao zitakazo msaidia kupelekea kutengeneza vitu vya thamani.

Tatizo sio mazingira yalivyo bali ni hile tafsiri inayozaliwa katika macho yako usipofumbuliwa huwezi sababisha matokeo, mathalani unaweza okota dhahabu na ukaitupa mtoni nawe ukawa na amani kabisa maana uliona kama jiwe lisiloweza kufanya jambo lolote na mwingine akaliokota katika mto na kuona ni dhahabu hatimaye likafanyika kuwa ukombozi wa maisha yake yote.

Macho yako yasipofumbuliwa nawe ukaona hata ushauriwe vipi kufanya jambo fulani utaona ni mateso tu na utaona hakuna la maana unalolifanya hapo.

Yakupasa kujua ukombozi wako uko katika kuona sio katika macho bali katika akili iliyojaa mwanga wa kesho uliobora.

Macho yako yakifumbuliwa katika kufanya jambo fulani hautahitaji msimamizi wala msukumo mwingine wowote.

Kuchoka wala kukata tamaa hakutakuwa ndani yako utaona unaweza kesho hata kama leo  haukufanikiwa.

Hali hii uwa unamuona Mungu kwa ukubwa sana kuliko jambo lolote unaloliona kama ni kikwazo kwako.

Haupaswi kuona mfano ili uweze kujitia moyo bali tayari nguvu ya kuendelea iko ndani yako na inaongezeka kadili ya magumu yanavyoongezeka nayo inaongezeka.

Utofauti wa watu wengi katika matokeo ni namna wanavyotafsiri mambo kwa jicho.

Huyu yuko hapa na yule yuko pale inategemea namna unavyoona na neema ya Mungu iliyo juu yake.

Haupaswi kuyaona mambo kikawaida yakupasa kuyaona mambo kwa jicho la pili ili uweze kujipata.

Mathalani, sio kila uchafu unausukuma mbali bali kuna aina ya uchafu unaweza pata wazo kupitia hapo unaweza pata mpenyo wako,kuna watu wamebadilisha maisha yao kwa kufanya taka kuwa kitu cha kufaa na hata kupata soko.

Ni wazi macho yako yasipofumbuliwa unawezapata nafasi na usiitumie Ipasavyo.

Hali hii ikikosekana kwako unaweza kujikuta una walaumu watu wengi na kuona wao ndio sababu ya wewe kushindwa kutoka hapo.

Macho yako yanapofumbuliwa unaweza kuiona fursa na kuiendea.

Barthomayo “ alipoona yesu anapita hakuacha fursa hii ipotee bali alitumia vizuri ndipo hatua nyingine ikazaliwa katika maisha yake” Ni lazima uone ili upate.

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.

 

Imeandaliwa na:

 

Cothey Nelson…………………………………………………………………………0764 018535

Ijumaa, 13 Machi 2026

AKILI NJEMA

 



Akili katika maisha ya mwanadamu imegawanyika katika sehemu tatu katika dhana ya kufikirika:

i. Akili katika hali ya kutegemea

ii. Akili katika hali ya kujitegemea

iii. Akili katika hali ya kutegemewa

Awa ni watu watatu tofauti wenye utendaji tofauti kabisa na upeo tofauti kabisa katika kuyakabili mambo/kuyaendea mambo.

Akili nayo inatabia ya kukua kutoka katika hali moja na kwenda hali nyingine ( ongezeko la ufahamu ).

Ni kama maisha ya mwanadamu uanza kwanza kwa kutegemea alafu ujikuta katika hali ya kujitegemea mwishowe anakabaliwa na majukumu ya kutegemewa hapa ndipo akili inabeba mzigo mzito.

Bila shaka usipokuwa makini unaweza kujikuta unakuwa mahali ambapo haukupaswa kuwa au haukutakiwa kuwa.

Kuna wakati akili yako isipotaka kujitegemea, mazingira yanaweza kutengeneza hali ambayo itailazimisha akili ianze kujitegemea japo mwanzoni kunakuwa na hali ya maumivu sawasawa na kuingizwa mahala ambapo hukutegemea kuwepo mpaka ukubaliane na mazingira unakuwa umeshaumia sana/vyakutosha ( mtu anapoenda uabuni kwa mara ya kwanza kusoma au kufanya kazi anakumbana na mazingira ambayo sio rafiki lakini baadae anawezakuyaelewa hayo mazingira ).

Tuangalie akili katika hali zake:

I. AKILI KATIKA HALI YA KUTEGEMEA

Ni hali ya kujua huwezi kusimama peke yako bila kushikwa mkono na mtu.

Ni sawasawa na biashara ambayo haiwezi kusimama yenyewe au kujiendesha bila usaidizi kutoka nje.

- Hali hii inapaswa kuwa ni hali ya kitambo na wala sio ya mwendelezo.

Usipokuwa makini unaweza kujikuta huko katika hali hii hata unapoingia miaka 50 na ukaona hali ya ushwari pasipo kujua hayo maisha hupaswi kukaa.

Ni maisha mazuri kimuonekano lakini ni maisha yanayo nyima pontetial yako kuonekana na kuwa faida kwa wengine ( uwezo wako wa kufanya mambo unakuwa ni mdogo au hauonekani )

- Katika hali hiii mwanamke au mwanaume anapoteza sifa ya kuwa katika ndoa, mazingira haya yanaondoa ubora wako kabisa.

Huwezi kunawiri katika akili hii

Ukiwa katika hali hii ukiachwa mahali utakutwa hapo hapo hata kama imebaki sehemu ndogo ya kufanikisha hilo jambo.

- Maisha ya utumwa yanazaliwa katika akili hii.

II. AKILI KATIKA HALI YA KUTEGEMEA

Hapa akili imeingizwa katika ulimwengu mgeni na hivyo akili imeanza kukubaliana na kutengenezwa.

Hichi ni kipindi cha kuanza kusimama mwenyewe kabla ujaanza kusimamisha wengine.

- Hiki ni kipindi ambacho unaanza kujitambua wewe ni nani hasa na unapaswa kufanya nini?

Ni kipindi ambacho kinawapa wakati mgumu  watu wengi kukuelewa kwa namna unavyoenenda.

- Kuna baadhi ya mambo yatakuwa mapya kwako na kwao na hivyo kukupelekea wao kukushangaa na wakati mwingine hata wewe kujishangaa.

Kuna mambo ulikuwa unayasikia sasa hapo wewe unaanza kuyashuhudia yakitokea katika maisha yako.

Kuna baadhi ya mambo ulikuwa unashangaa kuona watu wanafanya/kusema sasa katika hali hii au hatua hii utaanza kujua sababu ya hayo kuwa hivyo.

- Unapaswa kuwa makini sana maana katika kipindi hiki unaweza kujenga hatma yako au kuharibu maana katika kujifunza mambo mageni unaweza kuharika badala kujengeka.

Hichi ni kipindi ambacho mfumo mzima wa maisha yako unaanza kubadilika kama ulikuwa unakaa sasa unaaza kusimama na hatimaye kutembea.

Nikipindi ambacho wewe binafsi unajipa nafasi kubwa katika kujitafakari.

- Kama ulikuwa na maono basi sasa unaanza hatua ya kwanza kuelekea kutimiza maono yako.

III. AKILI KATIKA HALI YA KUTEGEMEWA

Sasa hapa akili yako inaanza kuyafanya maisha yako kuishi kwa ajili ya wengine.

- Katika hatua hii gharama kubwa unaingia sio kwa ajili yako bali kwa wale wanaokuzunguka.

Hapa ndipo hata kama mwili wako hauko sawa itakulazimu kusimama na kufanya au akili yako itakuambia jitie nguvu uende maana wako watu wanakutegemea ili maisha yao yaende.

- Hapa mtu anaweza kuwa na kikao cha peke yake hata akiwa barabarani.

Endapo utashindwa kutimiza majukumu kwa wale watakao kuzunguka huweza kuchukua maamuzi ambayo watu wanaweza kushangaa na kuanza kujiuliza hivi ni yeye yule tunaye mfahamu au mwingine.

Ni kipindi ambacho unahitaji kujielewa sana ama kuwa na akili ya ukomavu .

Ni hapa kama una makosa ukiyafanya unaweza kuhisi dunia nzima wanakuzomea, ama kuhisi huko uchi mbele za watu.

Ni akili ambayo unapaswa kuwa nayo katika kuwafanyia mema kwa wale wanaokutegemea kama wewe ulivyo fanyiwa mema ( sio wote ) na hatimaye ukawa pale ulipo, ( hata kama ujapata nafasi ya kufanyiwa mema lakini bado unayo nafasi ya kuwafanyia mema wale wakupendao )

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

 

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson………………………………………………………………………………..0764 018535

Ijumaa, 13 Februari 2026

USIOGOPE


 

Moja ya neno nzuri ambalo linawapa hatua mpya au kuendelea zaidi pindi watu wanapolisikia ni neno USIOGOPE.

Japo kuna wakati unaweza kukosa nguvu katika mambo yanayokukabili, unaweza kuona  yanakuzidi nguvu lakini hata hapo unaambiwa USIOGOPE inakuwa sawasawa na gari lililokosa/lililopoteza mwelekeo kwa sababu ya kukosa brake likielekea kwenye maporomoko lakini hata katika hali hiyo unaambiwa usiogope, japo kuna wakati unaweza kupoteza maana halisi ya hili neno maana  unaweza kuona kama  unakikabili kifo chako.

Duniani kuna mambo mengi yanayotisha na kuogopwa sana sio yale yanayoendelea katika maisha yako binafsi tu bali hata yale yanayoendelea katika jamii yako ama duniani.

Unapaswa kujua neno pekee linaloweza kumwingiza Mungu katika utendaji ni kutoogopa ambalo linakua zao kuamini.

Hauwezi kushindwa kuogopa katika mazingira yanayotaka uyaogope isipokuwa umejua kwanini usiogope au umepata uhakika na kuwa salama katika hayo mazingira.

Moja ya mateso mengi kwa watu ni zao la kuogopa, na kuogopa ni rafiki wa hofu.

Wako watu wameshindwa kubeba ujauzito kwasababu ya hofu, kwa kuhofia je! Atakuwa salama kweli au hata hatarisha maisha yake.

Wako wameshindwa kufanya mambo makubwa kwa sababu ya hofu, nafasi zinaweza kuja na kukupa hatua nyingine au kukupa ushuhuda lakini unaweza kushindwa kufanya kwa sababu unahofia je ikishindwa kufanikiwa je! Nitakuwa mgeni wa nani? Mathalani kuna nafasi zinatokea unatakiwa uwekeze hela zako nawe unazo lakini unahisi je! Zisizoporudi nitakuwa katika nafasi ipi?

Kuthubutu kunaweza kukufanya ufanye mambo makubwa au uwe katika namna nyingine lakini hofu imekuwa kikwazo cha wewe kufika hapo.

Yakupasa kujua kwamba hakuna mabadiliko yasiyokuwa na gharama hivyo unavyoogopa kufanya mabadiliko kwa kuhofia gharama utakazoingia bila shaka kuvuka ng’ambo inaweza kuwa ni vigumu.

Wako watu wameogopa kuingia huko kutokana na yale yanayoendelea katika jamii manyanyaso, mateso na magonjwa yanayozaliwa kutokana na hali hizo.

Tambua usipobadilika maisha yako hayawezi kubadilika ufahamu wako utakuwekea mipaka.

Mambo mengi yanategemea ni utulivu wa akili yako na namna unavyomtanguliza Mungu pasipo kuweka matamanio yako mbele.

Japo kuwa nyuki wanang’ata na wanaweza kuua lakini watu hawaachi kulima asali.

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

 

Imeandaliwa na:

 

Cothey Nelson……………………………………………………………………………….0764 018535