Ijumaa, 24 Julai 2026

KOSA LANGU

 



Hatia yoyote katika maisha ya mtu ni matokeo ya makosa aliyoyafanya kwa kujua au kutokujua.

Na kila kosa lina ishi na madhara yake haijalishi ni madogo au makubwa!

Na baada ya kufanya kosa kinachoendelea kukutesa sio kosa tena bali ni hile hatia ( madhara ) inayo tawala nafsi yako.

Na hatia inapokuwa ndani yako inapelekea kujihukumu na kujiweka mahali pa makosa.

Ni muhimu utambue kuwa maisha ya hatia yanakupa maisha yake na sio maisha yako utaanza kuishi sawa na hatia itakavyo kuongoza na sio kama unavyoona au unavyotaka.

Moja ya matokeo ya hatia ujasiri upotea kama sio kupungua, ukweli inawezekana hilo kosa hakuna aliyekuona lakini nafsi yako inapoaza kukuhukumu hapo uzito katika utendaji uanza kuchukua nafasi katika moyo wako.

Bila shaka katika dunia ya leo moja ya tatizo linalosumbua katika maisha ya watu ni hatia iliyo ndani ya maisha ya mtu inayomtawala na kuyaendesha maisha yake.

Hali hii isipofanyiwa utatuzi wa haraka unaweza kupelekea mtu kuwa na tatizo la akili. ( afya ya akili )

Zipo hatia zinazozalishwa na vitu mbalimbali mathalani, mikopo iliyoshindwa kulipwa na kupelekea kupoteza mali zake alizo chuma kwa tabu inawezekana ni mashamba,  nyumba au ofisi.

Maswali mengi yanakuwa hivi kwanini nilikopa na kwanini nimeshindwa kurudisha mkopo wa watu? Unaweza kuwaza siku nzima na bado ukakosa jibu sahihi.

Pia ziko hatia zinazozaliwa katika mahusiano hasa mahusiano ya ndoa , zipo ndoa zilizo dumu mwezi mmoja tu na baada ya hapo majuto na kujilaumu imekuwa ndio maisha ya kawaida na kusema kwanini nilikubali kuolewa na huyu na sio yule na mwingine anaweza juta kwa kusema sijui nini kilicho nifanya nimuoe huyu maana kama sio huyu nisingekuwa katika dimbwi hili lenye kina kisichokuwa na mwisho.

Mara nyingi maamuzi mengi yanayozaliwa na moyo uliojaa hatia na maumivu makali pamoja na majuto uweza kupelekea hata kifo.

Pia ziko hatia zinazotokana na watu wakaribu ( maraiki au ndugu ) pindi unapo msaidia katika jambo fulani kisha naye anakugeuka mathalani ulipambana kumtafutia nafasi hapo ofisini kwenu baada ya kupata kazi unakuta yeye ndiye anatengeneza mpango wa wewe kufukuzwa kazi, hali hiyo inaweza kuzalisha maumivu na uchungu usio isha.

Unapaswa kujua hatia haipo kwa ajili ya kukutesa bali ni kama alama unayokaa kwa kusudi maalum.

Hatia isikufanye kuona mambo sasa hayawezekani kana kwamba maji yame mwagika hivyo hauwezi kuyazoa tena.

Unapaswa kujua hatia ni msingi mzuri wa kufanya jambo ulilolifanya na kulitenda likutengenezee uwanja wa kuwa bora kesho kuliko leo.

Haupaswi kuruhusu hatia ikupelekee kuishi maisha ya hofu au ya mateso hali hiyo utakuwa umeruhusu mwenyewe lakini hilo sio lengo la kufanya ujisikie hatia.

Maisha mapya yapo tayari kuzaliwa katika hali hiyo ya hatia na sio kuharibu maisha yako uone kwamba umefika mwisho.

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.

 

Imeandaliwa na:

 

Cothey  Nelson………………………………………………………………………..0764 018535

Ijumaa, 10 Julai 2026

YAACHE MAISHA YAKO AKUPE MAISHA YAKE

 



Hakuna kitu muhimu kwa mtu kama maisha yake binafsi.

Kwa kuwa jukumu la maisha ni jukumu la mtu binafsi, hivyo kila mtu ushughulika sana kufanya maisha yake ya leo yawe bora kesho.

Hivyo sio jambo la kushangaza kuona mtu akipambana kuhakikisha maisha yake yanakuwa salama.

Japo kuna wakati tunajisahau kuwa hayo maisha unayoishi kuna MUNGU amekupa uyaishi na yeye akitaka usiendelee kuishi hakuna atakayezuia kusudi/ mpango wake labda atake mwenyewe katika mapenzi yake.

Ni kweli unayo nafasi ya kuwaza vizuri na mipango thabiti juu ya maisha yako lakini kukamilisha hayo vizuri, mbali na jitihada zako pia kuna hitaji neema ya Mungu ili kukupa kibali cha wewe kuyafikia yale uliyopaswa kuwa nayo.

Lakini Mungu anatambua unahitaji akupe maisha yake ili uishi maana katika maisha yako tu huwezi kujua mwelekeo unapaswa kuelekea.

Kuwa na mchakato wa kuyatengeneza maisha yako ukweli ni jukumu lako  ili usiwe na lawama juu ya watu wengine wasio husika na maisha yako bali ni muhimu utambue kuna nafasi ya Mungu katika kukupatia mema ili uweze kuyakamilisha yale unayopaswa kuyafanya.

 

Karibu!

“ Yaache maisha yako akupe maisha yake”

Sio wakati wote yale unayoyawaza na kuyafikiria mchana na usiku juu ya maisha yako yanaweza kuwa na taswira sahihi ya wewe ulipaswa kuyaishi.

“ Maisha yake” ni yale maisha ambao ulitengenezwa kuwa ( original yake ) yeye anajua kwanini upo.

Unaporudi kwenye asili yako na Mungu anarudisha mema yake juu yako ili kukutambulisha katika nafasi yako katika utukufu wake wa ajabu.

Maisha hayabebwi na vitu vinavyoonekana kwa macho kuwa vinapendeza na vinavyovutia bali yamebeba vitu visivyoonekana vilivyowekwa ndani yako hivi vitu vikiwa hai na kukuta uhai wa mwili unakuwa katika hali yake njema yaani ndani ya asili yake.

Unaweza ukatengeneza gari na ukaweka kifaa au kubadilisha kifaa kibovu na kuweka kizima na kweli gari linaweza kwenda lakini mwendo wake unaweza usiwe sawa kama kukiweka kifaa halisi ambacho kilitakiwa kuwa hapo maana gari linarudi katika asili yake.

Unahitaji kumjua  Mungu ili usiweze kupingana na Mungu pale anapotaka kukurudisha katika asili yako, kuwa mnyenyekevu na utaona matokeo yake.

Ni kweli mtu unaweza kuishi katika asili yake katika mazingira yasiyo sawa mathalani: mwandishi, mchungaji n.k ukafanya jambo nje ya neema ya Mungu ( tofauti na asili yako ) sawa na unachokiona kwa macho yako pasipo kuangalia mwenye asili yake aliyoyaweka ndani yako kama anakufurahia.

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

 

Imeandaliwa na:

 

Cothey  Nelson……………………………………………………………………………….0764 018535

Ijumaa, 3 Aprili 2026

MACHO YAKO YAFUMBULIWE

 

Ili uone kitu zaidi unachokiona au uone kile ambacho wengine hawakioni unahitaji mwanga katika macho yako.

huweze kuona kile kisichokuwa na picha/muonekano mzuri kuwa na muonekano mzuri wa kuvutia ( kisichoonekana ili kionekane ).

Vile ulivyo inategemea kiasi cha jicho lako lilivyofunguliwa kuona hivyo kadili unavyofunguliwa ndivyo unavyoona.

Ukifumbuliwa kidogo utaona kidogo na ukifumbuliwa sana utaona sana.

Kuna hatma kubwa zimefichwa katika kuona.

Ni kama watu wawili wanapoutazama mti wanapata tafsiri tofauti: mmoja anapouangalia anaweza kuona kuni nzuri zitakazo mfaa katika upishi wake na mwingine anapoangalia akaona mbao zitakazo msaidia kupelekea kutengeneza vitu vya thamani.

Tatizo sio mazingira yalivyo bali ni hile tafsiri inayozaliwa katika macho yako usipofumbuliwa huwezi sababisha matokeo, mathalani unaweza okota dhahabu na ukaitupa mtoni nawe ukawa na amani kabisa maana uliona kama jiwe lisiloweza kufanya jambo lolote na mwingine akaliokota katika mto na kuona ni dhahabu hatimaye likafanyika kuwa ukombozi wa maisha yake yote.

Macho yako yasipofumbuliwa nawe ukaona hata ushauriwe vipi kufanya jambo fulani utaona ni mateso tu na utaona hakuna la maana unalolifanya hapo.

Yakupasa kujua ukombozi wako uko katika kuona sio katika macho bali katika akili iliyojaa mwanga wa kesho uliobora.

Macho yako yakifumbuliwa katika kufanya jambo fulani hautahitaji msimamizi wala msukumo mwingine wowote.

Kuchoka wala kukata tamaa hakutakuwa ndani yako utaona unaweza kesho hata kama leo  haukufanikiwa.

Hali hii uwa unamuona Mungu kwa ukubwa sana kuliko jambo lolote unaloliona kama ni kikwazo kwako.

Haupaswi kuona mfano ili uweze kujitia moyo bali tayari nguvu ya kuendelea iko ndani yako na inaongezeka kadili ya magumu yanavyoongezeka nayo inaongezeka.

Utofauti wa watu wengi katika matokeo ni namna wanavyotafsiri mambo kwa jicho.

Huyu yuko hapa na yule yuko pale inategemea namna unavyoona na neema ya Mungu iliyo juu yake.

Haupaswi kuyaona mambo kikawaida yakupasa kuyaona mambo kwa jicho la pili ili uweze kujipata.

Mathalani, sio kila uchafu unausukuma mbali bali kuna aina ya uchafu unaweza pata wazo kupitia hapo unaweza pata mpenyo wako,kuna watu wamebadilisha maisha yao kwa kufanya taka kuwa kitu cha kufaa na hata kupata soko.

Ni wazi macho yako yasipofumbuliwa unawezapata nafasi na usiitumie Ipasavyo.

Hali hii ikikosekana kwako unaweza kujikuta una walaumu watu wengi na kuona wao ndio sababu ya wewe kushindwa kutoka hapo.

Macho yako yanapofumbuliwa unaweza kuiona fursa na kuiendea.

Barthomayo “ alipoona yesu anapita hakuacha fursa hii ipotee bali alitumia vizuri ndipo hatua nyingine ikazaliwa katika maisha yake” Ni lazima uone ili upate.

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA.

 

Imeandaliwa na:

 

Cothey Nelson…………………………………………………………………………0764 018535