NITAIJUA
BAADAE
Hakuna
kitu kizuri kama kujua! Japo uzuri wa kujua unakamilika pale unapo jua na
matokeo yake unapoyaona!
Kila
mtu utamani kuwa na kesho nzuri lakini shida inakuja pale namna ya kuifikia
hiyo kesho iliyo ndoto yako( iliyo beba kiu na shauku ya moyo wako)……… unaweza
kukuta mwanafunzi alikuwa ana mipango yake labda baadae awe rubani, wakili,
engineer, muhasibu, mwalimu na hata taaluma nyingine lakini mchakato wake unaweza kubadilisha hiyo ndoto yake kutokana
na matokeo ya kidato cha nne au cha sita kutokidhi vigezo vya kumwezesha kusoma
masomo Fulani au taaluma aliyokusudia hama maamuzi binafsi, ukakuta muhasibu
akawa mwalimu hama mwalimu akawa muhasibu,
Naam
imekuwa ni rahisi kwa mtu kunung’unika, kughairi, kukasirika kwa jambo
analolitegemea kushindwa kufanyika kwa muda alio upanga au namna alivyotaka
mathalani unaweza kukuta mtu anaweza kujisikia vibaya kwa kuachwa na ndege na
pindi akiwa kituoni analia na kusikitika pamoja na kumlaumu mtu anayedhani aliyesababisha
hayo yatokee lakini ghafla akasikia ripoti kuwa ile ndege imelipuka…. Bila shaka
ataondoka taratibu na kwenda sehemu ya mapumziko huku akimshukuru
Mungu…..NITAIJUA BAADAE!
Wako
watu wamegombana na kupelekea hata kuachana na wazazi wao, marafiki zao haya
yote yanawezekana ni baada ya kutoa majibu binafsi katika kila tendo
analofanyiwa hama analo hisi anafanyiwa na pindi ikatokea kuwa tofauti na
uhalisia wa mawazo yake baadae ikapelekea majuto ya kudumu.
Japo ni muhimu kutambua jambo kwanini hili
limekuwa hivi au limekuwa vile lakini sio lazima kujisumbua sana ili mradi ujue
tu! Unaweza kukuta mtu anasema kila jambo linalo nitokea uwa sili, silali mpaka
nijue kinaga ubaga lakini yako mengi unahitaji ukubali tu kuwa UTAIJUA BAADAE
SABABU YAKUTOKEA KWAKE.
Upaswi
kukosa raha kwa jambo ambalo alina utatuzi uliobora au wenye tija katika ufalme
wa Mungu maana huyo ndio ustawi katika maisha yako,
Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na
zijulikane na Mungu.
Kuwa na wasiwasi kama hatima yako imeshikwa na watu wengine lakini
kama iko mikononi mwa Mungu huna haja ya
kujitetea zaidi wewe simama katika nafasi yako, japo kuwa yako mengine
yataonekana ni magumu kunyamaza kimya tambua kuyaruhusu yachanganye akili yako
kunaweza kupelekea kuharibu hatima yako.
Kuongea sana akupelekei usalama wako kuwa mkubwa bali ufumbuzi
sahihi upelekea usalama wako wan je na hata wa ndani kuwa wakutosha na kufanya
uzidi kuwa bora katika utatuzi wako katika yote yaliyopo na yatakayo kuja.
INAITWA SIKU!BARIKIWA.
Imeandaliwa na:
Cothey Nelson………………………………….0764
018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni