Jumanne, 14 Februari 2017

UBORA WA MTU



UBORA WA MTU


Kuna dhana mbili zinazo kinzana kama sio kushabiriana UBORA /UMUHIMU

Ukweli ni makosa sana kufananisha umuhimu na ubora japo wakati mwingine kutokana ubora wa mtu uweza kupelekea umuhimu wake, kwa maana kama hakuna uhitaji wake/ umuhimu wake basi watu uweza kuona hapo hakuna UBORA wakati ubora siku zote uko ndani yake lakini umuhimu upo penye uhitaji tu.

Japo kuwa ubora wa mtu anakuwa nao mtu ndani yake lakini umuhimu wa mtu unaoneka pale atakapoonyesha utendaji wake, na wakati mwingine umuhimu wa kitu uonekana pale kinapokosekana, kwa hivyo yale mambo yake yanapokosa mbadala basi hapo ndipo uona nafasi yake.

Nipende kusema kuna wakati UMIHIMU wa kitu unaweza isha lakini sio ubora uliondani, kwakua ubora ni kitu alichokiweka Mungu ndani ya mtu kwa faida yake,

Ubora wa mtu ahuonekana katika muonekano wa mtu japo umuhimu wa mtu unaweza kutokana na muonekano mathalani mashindano ya urembo, model uwa wanapenda watu wenye umbo fulani lakini huo sio UBORA wa mtu.

Ubora wa mtu tunauona kwa Mungu pale alipo amua kumuachilia mwanae kipenzi kwa ajili ya mwanadamu!

UBORA WA MTU!

Kama mzazi pindi anapomwangalia mtoto wake uwa siku zote anamuona kuwa katika UBORA WAKE ( kwa mzazi mwenye akili) na sio kwa umuhimu wake, maana anajivunia yeye anajisifia yeye na fahari yake imebebwa na yeye,

Ndo mana Mungu alionyesha THAMANI/UBORA wa manadamu kwa kumtoa kipenzi chake, kwa maana rahisi tu kuwa Mungu alitoa kipenzi chake kwa ajili ya wapenzi wake, mwanadamu ulivyo kuwa bora ili mlazimu atoe kilicho bora,

Japo katika dunia ya sasa ubora wa mtu umekuwa ukichukuliwa katika hali isiyo sawa ndomana watu kuutoa uhai wa mwenzake kwa ajili ya maslai binafsi hawaoni shida, kumtoa kasoro mtu kana kwamba anaweza kumrekebisha, unaweza kukuta mtu anasema”mwangalie anamacho makubwa kama mguu wa tembo asingekuwa anayatoa maana yanatisha” mtu anaongea kwa ujasiri tena pengine wakitiana ujinga na mwenzao huku wanacheka kwa kebei.

Unaweza kukuta mtu anasema”huyu jamaa ombaomba yaani akikuona lazima akubomu ingefaa naye awe mgogo na aende Dodoma” watu wanasema tu kwa kuwa wamepewa kinywa cha kusema kwa hiyo wana kitumia vile wanavyoona na wala sio kama wanavyopaswa,

Pia unaweza kuta watu wanasema “ king’ang’anizi kaja yani akishiria jambo lake hata la uongo yani huyu mbishi  yani ruba anasubiri kwa ung’ang’anizi wake bora angekuwa super glue ingejulikana moja, mangi angeuza iishe”

Yako mengi lakini watu wako huru kana kwamba wanamjua mwanadamu kinagaubaga hama walikaa na Mungu wakati anamtengeza mtu au huyo jirani yake,

Marko 12:31 Na ya pili ndiyo hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.

Biblia imekosa lugha nzuri yakueleza ikasema kama unavyojiona na kujipenda, kujithamini basi fanya hivyo kwa mtu yeyote pasipo kujali unamjua hama umjui,

1 Yohana 4:20 Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.

Lazima ujue hatima umeshika na wewe ila Mungu ndio muamuzi, sio kila hali aliyonayo mtu binafsi anaifurahia laiti ungeuona usiku wake namna macho yake yanavyolowesha mashuka yake usinge thubutu kuwaza tofauti na namna unavyopaswa kuwaza,

UBORA WAKO NA WAKE NI SIRI YA MUNGU!

ANAITWA MUNGU! BARIKIWA.

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson…………………………………………………..0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni