UTAMBULISHO
WA KIMBINGU
Swala sio utambulisho
tu! bali unatambulishwaje? Wewe kama nani na katika hadhi unayostahili!
Ndani ya dunia ya sasa
kumekuwa na shida sana kwa baadhi ya watu kuwepo mahali Fulani alafu
wasitambulishwe kama anavyotaka japo pia wako watu ambao hawana shida sana
katika utambulisho,.wako watu wanaghaili kwenda mahali Fulani au kujuta kwa
sababu ya kutotambulishwa vile wanavyotaka,wako watu wanaanza kuchukiana na
kisilani kisa ametambulishwa ki kawaida sana kwahiyo mojamoja ufikiri ni dharau.
Uko urafiki na kushirikiana
kumekuja pale tu baada ya mtu kutambulishwa vizuri na pengine hata kupewa sifa
ambayo hakustahili na hivyo kujenga undugu na mashirikiano ya muda kulingana na
shughuli yenyewe, japo kutambulishwa hakuongezi hela wala hakupunguzi hela
lakini ni kitu cha kawaida tu ni kama kitu cha kutambulika na sio maana
nyingine ukiwa katika hali hii basi kama umesahaulika kutambulishwa bado
utakuwa na amani kwa kua unajua kama binadamu ni hali ya kawaida kupitiwa
lakini kisiwe chanzo cha maamuzi yasiyostahili.
Kila utambulisho
unakazi yake katika mazingira husika,na ina aminika kila hadhi ina heshima yake
mathalani bosi na mfanyakazi kila mtu anautambulisho wake na unanafasi yake,iko
raha ya dunia pindi dunia inapokutambulisha katika nafasi mbalimbali mathalani
rais,waziri,boss na hata manager kuna haki utazikosana kama usipotambulishwa
katika nafasi unayostahili kwakua heshima ya dunia utaikosa lakini endapo
ukatambulishwa basi utayapata yale unayopaswa kuyapata.
Ni kitu kizuri sana kwa
mtu anayestahili heshima basi na apewe heshima kutokana na hadhi aliyokuwa nayo.
UTAMBULISHO
WA KIMBINGU
Kuna utambulisho ambao
unatisha na unashangaza umebebwa na umesimamiwa na Mungu mwenyewe na sauti yake
inapotokea ardhi na mbingu vinatia muhuri kuwa vinashikilia katika kutekeleza
katika Mungu alichokisema, huu ni utambulisho wa kudumu kwani utambulisho
wowote unaweza kuwepo na kuonekana kama kama yeye aliye kutambulisha akiwepo
lakini utambulisho wa kimbingu ni utambulisho ambao hauna mwisho wala kikomo.
Uwezi kutambulishwa
bila kujitambua!!!
Mungu akujidhihirisha kwa watu ili mradi walikuwa
wanamtumikia bali yeye ujidhihirisha kwa Yule ambaye anatembea katika nafasi
yake kikamilifu.
Paulo
anasema……….Mungu alipoona vema kumdhihirisha mwanawe ndani yangu!
Haya aliyasema akiwa ameshakubali wito wake na
kuanza kutendea kazi na hivyo akaona namna Mungu alivyo jidhihirisha katika
utendaji wake wote na hakuna aliloshindwa.
Lazima utambue na nafasi yake kwanza na kuipa nafasi
katika utendaji wa hiyo na nafasi ili Mungu achilie kitu ambacho
kitaadhihirisha kile unachofanya sio kwa ajili yako bali ni Mungu mwenyewe
anahusika hivyo atajidhihirisha kujionyesha.
Watu wengi wanatumia muda mwingi kutamani na kuiga
na kujifanya kuwa sasa Mungu amejidhihirisha kwao lakini jua kwamba halisi na
kisicho halisi kitajulikana tu baada ya muda Fulani, kwa kilicho halisi
kitadumu kwakua ndicho kilichopo na kitakuwepo….kwa kusema hivi ni sema kwamba
udhihirisho unajitosheleza na walio rohoni tu ndio watakao utambua.
Wako watu wanapopata nafasi za juu kazini wanafikiri
Mungu ame wakumbuka hivyo kuonyesha kuwa Mungu amejitambulisha kwao lakini
mwisho watu hao wamejikuta wakitembea na bosi zao na mwisho kuwa mbaya zaidi
mathalani familia zao kuvunjika na magonjwa kushamiri katika miili yao.( sio
kila jambo jema linalokuja kwako limebeba hatma njema katika maisha yako)
Lakini utambilisho wa mbingu hauna hatima mbaya…..
kwani umejaa manufaa ya rohoni na mwilini kwa ukamilifu………..na hautaji
ujipendekeze ili ujidhihirisha bali ni wewe kutembea katika nafasi yako
aliyokupa halafu yeye atakutambulisha tu!
Imeandaliwa
na ;
Cothey Nelson………………………………………..0764 018535
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni