Ijumaa, 1 Machi 2024

UBORA WA AKILI YAKO UTAKUMBULISHA:

 



Moja ya shukrani ambayo mwanadamu anayotakiwa kumpa Mungu ni kupewa akili inayomtambulisha kama binadamu, kwakuwa amemuumba kisha akampa akili ambayo inaweza kumsaidia kumtambulisha na yeye kujitambua,

Ni kweli kila kiumbe kimepewa akili ya namna yake mathalani mnyama ana akili zake, ndege na wanadudu wana akili zao na moja ya kazi kubwa ya akili ni kumuongoza mtu katika kuamua nini afanye na nini asifanye.

Kwa ujumla hakuna mtu asiye na akili bali utegemea matumizi ya mtu katika hiyo akili katika matumizi bora au mazuri na hapo anakuwa wa faida katika jamii lakini kwa matumizi mabaya basi hapo anakuwa janga  katika jamii yake.

Japo darasani ni lazima atokee mwanafunzi wa kwanza na mwisho lakini sio kweli kuwa mwanafunzi aliyekuwa wa mwisho basi hana akili kama wengine wasemavyo na kuamini atakuwa wa mwisho kila kitu.

Kila mtu anayo nafasi ya kuifanya akili yake kuwa ni kitu bora chenye manufaa kwake na kwa jamii yake.

Unapaswa kujua kuwa Mungu alikuamini ndo mana akakupa hiyo akili haijalishi unaielewa au hauielewi.

Lakini Mungu amekupa hiyo akili akijua utoshelevu wako utazaliwa na hiyo akili kupitia yeye!

Ukiitumia hiyo akili vizuri kwa hakika utaifurahia hiyo hatua uliyopo au unayoelekea mathalani ndege kuku yeye ufurahia kila kitu anachokifanya hatakama kesho atachinjwa lakini yeye uhakikisha leo yake ameitumia vizuri tena katika kiwango kikubwa cha akili yake.

Ni kweli hauwezi kuwa wa maana kama ujatambua matumizi sahihi ya akili yako,

Ni muhimu utambue ndani ya akili kuna kuona kule/pale ulipo au kule unakoelekea kunahitaji nini japo wakati mwingine unaweza usipate njia sahihi ya kufika hapo lakini tambua Mungu ameachilia hiyo neema ya kufika.

Kwa kiasi kikubwa unapomuona mtu yupo katika hatua njema/nzuri  ( nje ya utajiri wa kipepo) bila shaka ujue hayo ni matokeo ya ubora wa akili yake, kwakuwa ubora wa akili unapodhihirika katika mwili ndipo hapo mnayaona hayo matokeo.

Tatizo linakuja pale unapotaka/unapoanza kuyataka mafanikio yake pasipo kujua ubora wa akili yake ni tofauti  na akili yako, kuna upekee wake uliosababisha kuwa hapo.

Ni kweli watu wote mnaweza kuwa wafanyabiashara wa mbao na watu wote mkafanikiwa inawezekana hawa wakafanikiwa kwa kuuza mbao nje ya nchi na wengine wakafanikiwa kwa kuuza mbao ndani ya nchi hivyo uonyesha upekee wao katika matumizi ya akili lakini katika kila mtu kwa ubora wake,

Naam ni ukweli usiopingika kuwa unaweza kujifunza kwa waliofanikiwa katika matumizi sahihi ya muda, bidii, uaminifu na mengine mengi lakini usipojifunza katika ubora wa utendaji wake uliozaliwa katika akili yake kwa maana huyo ni yeye sawa na upekee ambao Mungu amemjalia,Lakini utakapoanza kutembea katika akili yake jua hapo utataka kuishi kama yeye anavyoishi na hapo ndipo makosa mengi yanaanza kutokea na hata kupelekea kuishia njiani!

Kwakua hauwezi kuishi kwenye akili ya mtu alafu ukajipata bali ukiishi kwenye akili ya Mungu hapo utajipata na kujua namna yako,

INAITWA KESHO! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………………………………………………………………..0764 018535

Ijumaa, 16 Februari 2024

UZURI WA HATUA MPYA:

 



Kwa mzazi mwenye mapenzi ya kweli kwa mwanae uwa anakuwa na furaha kubwa katika kila mabadiliko yanayofanyika katika ukuaji wa mwanae mathalani kutoka hatua ya kulala kuanza hatua ya kukaa….na moja ya hatua inayompa furaha mzazi kuona mwanae ameanza kupiga hatua au kutembea, kwani hapo anaweza kuwa msaidizi wa mahitaji madogo madogo kwake kama vile kumtuma akachukue kitu fulani ndani ya nyumba hadi dukani.

Naam hatua mpya ni shauku ya waliowengi kwa maana inaaminika katika hatua mpya kuna maongezeko, pia tunaweza sema kama uzuri wa kujifungua japo kuna maumivu lakini tunaita ni uzuri kwa sababu ya matokeo yake, kupakata mwana…………na heshima katika jamii inayokuzunguka.

Ni kama mlizi anavyoingojea asubuhi kwa hali ya shauku ndivyo ilivyo kwa mtu anayengojea hatua inayofuata kwa makamio yote.

Ni kama uzuri wa kutimiza ndoto yako ambayo ulikuwa unaitamani siku nyingi, inapotimia inageuza siku yako na kuwa hali nyingine iliyo njema.

Hatua ya juu au mpya ni kitu kinachofurahiwa na kupendwa na watu wengi kwa kuwa wanaamini katika hatua mpya uweza kuamini hadhi zao na mambo mengine uweza kubadilika.

Ni kama mwanamke anavyotamani kupakata mtoto na wakati akitambua kipindi cha kujifungua ni kuweka maisha yake rehani lakini inabidi akubaliane nayo kwasababu ndio hatua ambayo jamii inataka aelekee huko kwa maana inaaminika kuwa baada ya ndoa ni furaha kuongezeka.

Ni kama mkulima akiwa na shauku ya kuona mavuno na kuyafurahia na ikiwa anatambua kuwa kuamua kulima ni kuweka fedha yake rehani kwa kuwa inaweza kukata na kumwacha katika ndoto isiyokucha na kubaki kujuta bora asingeamua kupanda au kuingia kwenye kilimo.

Bila shaka hatua mpya ni jambo zuri linaloleta furaha kwa mtu mmoja na familia pamoja na ukoo kwa ujumla, kwakuwa wana amini kwamba kama mmoja akitoka katika kufanikiwa basi ukoo utakuwa na sehemu ya kupumulia au unafuu.

Niseme tu kwenda hatua mpya sio jambo la mchezo au la kawaida kuna hali unaweza pitia  hata usijue mara ya mwisho kulala usingizi ilikuwa lini maana inawezekana kipindi hicho kikasababisha hali ya kukosa utulivu wa akili na mwili kwa kiasi kikubwa.

Unapotaka kwenda hatua mpya ukaangalia mchakato wake usipokuwa na dhamira ya dhati unaweza kukuta umeghairisha kuingia katika hatua mpya na sio kwamba upendi hatua mpya bali ni ugumu wa mchakato unaonekana katika akili yako.

“ petro alipoamua kutembea juu ya maji alipoangalia mawimbi shaka ikaingia ndani yake na hatimaye akaanza kuzama……….”

Mathayo 14:26 Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu.

 27 Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope.

 28 Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.

 29 Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu.

 30 Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe.

 31 Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?

Hatua mpya unaweza kuifananisha na ng’ambo iliyojaa mema kwa ajili yako lakini kuna mto inabidi uogelee ili ufike ng’ambo na ndani kuna mamba wa kali lakini kwa namna yoyote inabdi upite katikati ya hao wanyama ili uyafikie yale mema yako yaliyo ng’ambo.

Akili ya mkulima uwa naipenda kwasbabu uwa inaangalia matokeo kabla ya kuangalia mchakato utakao sababisha matokeo hali hiyo inafanya kuukabili mchakato wote katika hali zote ugumu na kujinyima ili mradi apate matokeo anayo yataka au yale aliyokuwa anayawaza na ikiwezekana hata zaidi ya yale aliyokuwa anayawaza.

Hauwezi kupata mavuno kama ujafuata mchakato mzima wa kukupelekea hayo mavuno, kama haupendi mchakato wake basi hauko tayari kupata mavuno, ni sawa sawa mwanafunzi anataka kupenda daraja la juu huku hayuko tayari kulipa gharama ya kusoma kwa bidii.

Ni shauku ya Mungu tuingie katika hatua mpya sio hatua ileile kwa kuwa unapodumu katika hatua ya awali kwa muda mwingi kuna baadhi ya mambo hutaweza kuyapata mpaka uingie katika hatua nyingine, kila hatua ina utukufu wake hivyo ili upate utukufu mwingine basi hakikisha unaingia katika hatua nyingine.

Isaiah 1:19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi;

Hatua mpya unaingia kwa kuikubali na kuitii sauti ya Mungu, pindi utakapo amua kuishi sawasawa na sauti yake pasipo kuangalia nini kinaendelea nawe au gharama utajikuta upo katika hatua nyingine wenye utukufu wake.

“ kama ukuweza kunizuiliwa mwanao……………..basi sasa kukubariki nitakubariki”

Mwanzo 22:16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,

 17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;

 

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………………………..0764 018535

Ijumaa, 26 Januari 2024

USIJIPINGE

 



Katika dunia tuliyonayo sasa, mambo mengi yanatokea yanakuwa yanaongeza maswali vichwani mwa watu baada ya kutoa majibu: katika dunia ya sasa kuna ongezeko kubwa la watu kujitoa uhai, kujijeruhi binafsi na matukio mengi ambayo kwa hali ya kawaida hautegemei binadamu wa kawaida kufanya hayo mambo lakini unakuta yanatokea na kuongezeka kila iitwayo leo,

Na wataalamu wengi wakifanya uchunguzi wanajikita katika kujua au kuhisi chanzo chake na kutoa utatuzi  wa mambo haya yanayo wakumba wanadamu lakini bado inakuwa sio tiba ya kudumu katika jamii husika.

Naam! Moja ya kitu ambacho binadamu wa kawaida/mwenye akili timamu hawezi kufanya ni kujipinga ingawa anaweza kujikuta katika hali hiyo kwa kujua au kuto kujua.

Kama mtu unaishi haijalishi una mjua Mungu au haumjui Mungu kuna wewe katika hali ya ndani na kuna wewe katika hali ya nje! Na vyote vinakukamilisha wewe au kutoa picha yako kwa jamii.

Kwa maana rahisi kuwa wewe ulivyo  hasa ( ulivyotengenezwa kuwa ) na vile unavyoona katika mtazamo wa akili baadaa ya kushawishiwa na macho yako.

Mathalani, unaweza kukuta wewe katika hali yako ya ndani wewe ni maalum kwa ajili ya kutengeneza vinyago na ukitengeneza moyo wako unakuwa burudani lakini ukakuta unaingia katika kucheza mziki hali hiyo ikakupa mpingano mkubwa katika hali ya ndani na ya nje na unaweza kufika  mahali hata kushindwa kujua kuwa unaendelea mbele au upo palepale/hapohapo.

Pia katika uwanja wa uimbaji kuna vitu vitatu: performer ( mchezaji ), singer ( muimbaji ), worshiper ( mwabudu ) hawa wote wanaweza kuwa katika uwanja wa uimbaji ( music industry ) lakini hawaingiliani na pindi ikatokea mchezaji akatamani kuimba na pindi atakapoanza kuimba utaona makosa mengi kwa mtu asiyekuwa na talanta hiyo na hata akashindwa kuimba katika katika kiwaango/namna anayotakiwa.

-          Japo mchezaji na mwimbaji wote hawa wanaweza kuwa waabudu katika namna zao.

Ni hatari sana pale utakapoishi maisha ya kujipinga ( kuwa/kufanya tofauti na ulivyopaswa kufanya ) kutokana na kuogopa watu au kuangalia maslahi yako zaidi na fursa inayoonekana na kujisahau wewe na uwezo ambao Mungu amekupa kutumika katika eneo gani,

-          Pindi ikatokea upingamizi katika jambo hilo unalolifanya lisilo na shikama na hatma yako bila shaka hautaweza kushinda hali hiyo hata kama ukipambana vipi.

Unaweza kukuta mtu ni mbobezi wa kutengeneza script lakini ukajikuta anaingia katika uigizaji au kucheza filamu ambayo hafiti eneo hilo bila shaka anaweza kuharibu au akapoteza mvuto wa hiyo filamu kwa kuwepo mtu ambaye akupaswa kuwepo hata kama yeye yuko kwenye industry kwa miaka mingapi?

-          Na tambua kuna baadhi ya watu wanahitaji maboresho au maelekezo ili waweze kuwa kitu bora au kizuri lakini ni kwa wale wenye hiyo talent sio kulazimisha talent.

Pia unaweza kukuta mtu mwenye kalama ya ufundishaji ( mwalimu ) akatamani kalama ya kutoa unabii bila shaka anaweza kujitahidi kuendana na wenye kalama ya unabii lakini muda si mrefu watu watatambua kuwa yeye hayuko na kalama ya unabii,

-          Moja dalili ya kufanya kitu kisichokuwa chako upelekea hali ya juu katika matumizi makubwa ya akili ya kuhakikisha unalinda unachokifanya na wala sio kukiboresha.

Kufanya kitu ambacho sio chako ni sawa na kuvaa nguo isiyokutosha vizuri muda wote utakuwa ujiamini.

Unapotumia muda mwingi kufanya kitu kisichokuwa chako ni matumizi mabaya ya muda, maana ingekuwa bora/vyema kutumia muda huo kukiboresha na kukikuza ( kwa kuongeza maarifa yahusiyo hiyo talanta iliyondani yako ).

Ni muhimu ujivumbue ili ujiishi na uone raha ya wewe kuwepo duniani, pia inasaidia kujua nafasi ya wengine na kuwawezesha wengine kufanya.

Unapofanya kitu ambacho ni chako bila shaka makosa yatakuwa madogo sana na hata kushindwa kuonekana machoni pa watu kwa ukubwa.

Kufanya kitu ambacho akikutambulishi wewe ni sawa na mtu anayetamani kuzama kwenye maji kwa muda mrefu na huku akiwa hana pumzi ya kutosha kumudu muda huo, hivyo atakapoanza hilo zoezi kwa muda mchache sana utakuta ameinua kichwa juu huku akihema kwa harakaharaka kama mtu aliyenusirika kufa.

Ni kusudi la Mungu usijipinge hata kama kile ulichopewa akina mvuto kuliko vingine bali ishi hapo maana kwa kuishi hapo unaweza kuyafurahia maisha yako na kumshukuru Mungu kwa kukuumba na kukuweka hapo.

INAITWA SIKU! BARIKIWA SANA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………………………………..0764 018535

Ijumaa, 7 Juni 2019

HAKUNA UGUMU CHINI YA MAONGOZI YAKE!



“ kuna ugumu wa kupenda lakini hakuna ugumu kwa kinachopendwa”!

Unaweza kufika marekani kwa namna nyingi! Mathalani unaweza fika marekani katika mawazo yako na marekani iliyo katika uhalisia wake ( ukifika )…..ghafla unaweza kuichukia kwa kutaka kuishi marekani iliyo katika akili yako ( raha & starehe, maisha ya kifahari na ubora wa vitu na mambo yake ) pasipo kupata muongozo sahihi ya namna ya kuishi uko…………ni wazi kitu hicho kupata uharibifu ni jambo lisilo kwepeka.

Ndomana mara nyingi unaponunua kitu, bidhaa au mali fulani uwa kuna muongozo unapewa “menu book “ au karatasi kuhusu namna sahihi ya kutumia kifaa hicho.

Hata hesabu ikiwa imefumbwa kiasi gani hata ikatoa muonekano wa ugumu katika kupata jibu lake endapo ukabaini kanuni yake au namna ya kuanza na kuanza kupata mwelekeo basi hapo ugumu unaanza kupotea machoni pako, mathalani kanuni ya kufanya hesabu “ MAGAZIJUTO”
Na kuna msemo watu wanasema “ hakuna mkate mgumu mbele ya chai”

Karibu!!!

Katika maisha ya wokovu, watu wengi wanaipenda kutokana na matunda yake unapodumu katika wokovu, furaha ya Mungu, ulinzi wa Mungu pamoja na uzima wa milele, lakini kati hali hiyo unaweza kukuta watu wa aina tatu:
i.                    Wanaoacha wokovu
ii.                  Waliokosa mwelekeo
iii.                Wanaoimarika katika wokovu.

Ni jambo la kushangaza sana pindi unapoona kitu chenye manufaa kiasi hicho wapo wanatamani kuacha wokovu.

Sio furaha ya mchungaji wala kanisa katika kupunguza idadi ya watu kanisani bali ni kuwaongeza ili ufalme wa Mungu uzidi kujengeka, lakini hali hii ikitokea utokea tu kulingana na uimara ulionao katika wokovu.

Mathayo 7:24………………………………………………………
“Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba”

Usiishi katika wokovu kwa namna yako huku ukifuata hisia, matamanio pamoja na miemko yako bali tamani kuishi katika wokovu na mleta wokovu. ( unapoishi marekani usipende kuishi vyovyote bali tamani kujua wenyeji wanaishije! Wanapaswa kuishi vipi ).

Wokovu unakuwa sio mgumu pindi utakapoishi katika maongezi yake kweli ( Roho mtakatifu ), maana yeye ndiye anajua namna sahihi ya kuishi pindi unapokuwa ndani ya wokovu mengine yote yanapita. (mbwembwe, ushawishi wa maneno na mengine yote uwa kuna wakati unafika yanakosa nguvu tena)

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………….. 0764 018535

Jumamosi, 6 Aprili 2019

LIACHE KUSUDI LIVUTE MAMBO YAKE:



Ni jambo la fahari kwa mtu pindi anapofanya jambo akatambua kwanini anafanya hivyo au jambo hilo! Na litakuwa ni jambo la kushangaza kwa mtu awe anatia bidii sana na uku asijue kwanini anafanya hivyo.

Ni ukweli usiopingika pindi utakapoamua kulitumikia kusudi basi haki inayoambatana na hilo kusudi udhihirika au uweza kulipata.

Na ni jambo linakuwa gumu pindi utakapoanza kulitumikia kusudi uku ukiwa na matarajio yako ambayo ayaletwi na kusudi mathalani mtu unaweza ukajikuta katika shughuli za uvuvi lakini itakuwa ngumu kama moja ya kusudi lako ni kuvua swala mkubwa badala ya samaki.

Unapolitumikia kusudi uku akili yako ina mtazamo wako mbali na kusudi lilivyo ni ngumu kudumu na hilo kusudi au kuendelea na kusudi mathalani utakuta mtu anajitoa sana katika shughuli fulani akitegemea labda atapata pesa lakini pindi inapokuwa kinyume na matarajio utoshangaa kesho katoa udhuru wa kutoendelea na shughuli hiyo.

Biblia inasema “ hakuna aendaye vitani kwa gharama zake mwenyewe “.
1 Wakorintho 9:7 Ni askari gani aendaye vitani wakati wo wote kwa gharama zake mwenyewe? Ni nani apandaye mizabibu asiyekula katika matunda yake? Au ni nani achungaye kundi, asiyekunywa katika maziwa ya kundi?

Kusudi lenyewe linajua linahitaji nini ili liweze kudhihirika kwa hiyo ni muhimu ulitambue hilo na utoe nafasi lenyewe liite yaliyo yake sio swala la utendaji wa akili yako usio na uvuvio wake.
Ni muhimu kutambua kusudi lenyewe linaona kuliko macho ya nyama yanayoona, linajua chimbuko lake na hatima yake.

Uwezi kuchoka kama ukikubaliana na kusudi katika yale unayoyataka, kwa maana lenyewe kusudi linajua uhitaji wake.

Usipende kuishi katika maslahi yako pindi unapolitumikia kusudi bali ishi kwa matakwa ya kusudi bila shaka lenyewe litakutunza kukuimarisha maana ndilo matokeo au makusudi yake pindi utakapoamua kuishi katika hilo.

Kama unahitaji kuona fahari na ustawi wa familia na ukoo pamoja na watoto bila kusahau na wajukuu wako basi hunabudi kulitumikia kusudi ambalo Mungu ameliweka ndani yako.
Uzuri wa kusudi “ ukilitumikia nalo litakutumikia ila ukiliacha litakubwaga mazima “!

Nje ya kusudi uwezi kuona fahari ya wewe kuwepo duniani, kitu pekee ambacho kilicho mshawishi Mungu akuruhusu uje duniani ni kwa sababu ya hilo kusudi mbali na hilo hakuna kitu kingine.

Usiwe mjuaji sana katika kusudi maana utalitumia kwa namna yako ( kulitaka likutumikie baada ya wewe kulitumikia ) kwakuwa lenyewe lilivyoachiliwa linamaelekezo yote bali wewe kuwa mnyenyekevu na umakini wa kulisikiliza hapo utakua salama.

“ kuyapenda maisha yako ni kulipenda kusudi lililowekwa ndani yako “

INAITWA SIKU! BARIKIWA.

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………….0764 018535