Ijumaa, 7 Juni 2019

HAKUNA UGUMU CHINI YA MAONGOZI YAKE!



“ kuna ugumu wa kupenda lakini hakuna ugumu kwa kinachopendwa”!

Unaweza kufika marekani kwa namna nyingi! Mathalani unaweza fika marekani katika mawazo yako na marekani iliyo katika uhalisia wake ( ukifika )…..ghafla unaweza kuichukia kwa kutaka kuishi marekani iliyo katika akili yako ( raha & starehe, maisha ya kifahari na ubora wa vitu na mambo yake ) pasipo kupata muongozo sahihi ya namna ya kuishi uko…………ni wazi kitu hicho kupata uharibifu ni jambo lisilo kwepeka.

Ndomana mara nyingi unaponunua kitu, bidhaa au mali fulani uwa kuna muongozo unapewa “menu book “ au karatasi kuhusu namna sahihi ya kutumia kifaa hicho.

Hata hesabu ikiwa imefumbwa kiasi gani hata ikatoa muonekano wa ugumu katika kupata jibu lake endapo ukabaini kanuni yake au namna ya kuanza na kuanza kupata mwelekeo basi hapo ugumu unaanza kupotea machoni pako, mathalani kanuni ya kufanya hesabu “ MAGAZIJUTO”
Na kuna msemo watu wanasema “ hakuna mkate mgumu mbele ya chai”

Karibu!!!

Katika maisha ya wokovu, watu wengi wanaipenda kutokana na matunda yake unapodumu katika wokovu, furaha ya Mungu, ulinzi wa Mungu pamoja na uzima wa milele, lakini kati hali hiyo unaweza kukuta watu wa aina tatu:
i.                    Wanaoacha wokovu
ii.                  Waliokosa mwelekeo
iii.                Wanaoimarika katika wokovu.

Ni jambo la kushangaza sana pindi unapoona kitu chenye manufaa kiasi hicho wapo wanatamani kuacha wokovu.

Sio furaha ya mchungaji wala kanisa katika kupunguza idadi ya watu kanisani bali ni kuwaongeza ili ufalme wa Mungu uzidi kujengeka, lakini hali hii ikitokea utokea tu kulingana na uimara ulionao katika wokovu.

Mathayo 7:24………………………………………………………
“Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba”

Usiishi katika wokovu kwa namna yako huku ukifuata hisia, matamanio pamoja na miemko yako bali tamani kuishi katika wokovu na mleta wokovu. ( unapoishi marekani usipende kuishi vyovyote bali tamani kujua wenyeji wanaishije! Wanapaswa kuishi vipi ).

Wokovu unakuwa sio mgumu pindi utakapoishi katika maongezi yake kweli ( Roho mtakatifu ), maana yeye ndiye anajua namna sahihi ya kuishi pindi unapokuwa ndani ya wokovu mengine yote yanapita. (mbwembwe, ushawishi wa maneno na mengine yote uwa kuna wakati unafika yanakosa nguvu tena)

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………….. 0764 018535