Jumamosi, 23 Novemba 2013

TATHMINI YAKO NA MUNGU




TATHMINI  NA  MUNGU

Unaishije na Mungu…..?

Namna unavyoishi na Mungu inaweza ikakusababishia baraka au laana.

TATHMINI hili sio jambo geni kwa watu wengi kwani ni jambo linalo fanyika katika mazingira na hatua mbalimbali mathalani ndani ya familia wanatathmini maisha yao kwa ujumla na kuona kesho yao ina mwanga mzuri na kama haina na nini kifanyike? Katika makampuni,kijamii na hata katika ngazi ya kitaifa pia ufanya tathimini kuupata mstakabali wa kesho.

Lakini leo ningependa tushirikiane katika kufanya tathmini ya pamoja kati Mungu na sisi (wanadamu), katika kufikia hapo yako mambo kadha kujiuliza au maswali machache yanayo pelekea au kuleta maana ya tathimini yenyewe?

a) Wewe ni nani kwake na yeye ni nani kwako?

b)Mungu ni kielelezo namba ngapi kwako (mnaishi maisha yenu au yana fanana na wengine)?

c)Ni kweli yeye anafurahia maisha nawe nawe unafurahia maisha naye?

d)Unajua vile ulivyo ni matokeo ya wewe unavyoishi na Mungu (utofauti wenu na mtu mwingine inategemea sana mnavyoishi na Mungu)?

e)Ni kweli ile nguvu iliyo ndani ya Mungu iko ndani yako (lazima wote mfanane)?

f)Ni kweli maisha unayoishi nae yanafanya aone maana ya kukupa siku nyingine kwa furaha?

g)Unafikiri kitu gani unmfanyia Mungu hata kuona ile kazi ya msalaba haikua bure anapata faraja kwa wewe kuona unafanya vitu amabavyo yeye angekuwepo angevifanya?

h)Unatambua wewe hauwezi fika bila yeye ila yeye anaweza pasipo wewe?
Anaweza kuyainua mawe usiyotarajia.

i)Unaitambua nafasi aliyo kupa Mungu na ile unayompa katika mawazo yako.

k)Unatambua kuwa wewe ndio mwenye wajibu wakufanya Mungu afurahi kupitia maisha yako.


Imeandaliwa na ;
                     Nelson, Cothey – 0764 018 535 or cotheyn@yahoo.com
                    Katiti, James       - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com


KILA LA KHERI…………..RAFIKI