Ijumaa, 14 Septemba 2018

SWALI LINAKOSA MAANA!




Kama binadamu uliopata neema kuingia katika mifumo mbalimbali ya elimu na kufanya mitihani, utakuwa ulishakutana na maswali katika mitihani yaliyokosewa au yasiyo na majibu!

Wakati mwingine swali lililokosewa uweza kurekebishwa ili liwe na MAANA au kubadilishwa na pengine kutoa alama za bure (free masks) ikiwa hilo swali alikujulikana mapema wakati wa mtihani ila baada ya kusahihishwa mtihani likagundulika.

Karibu!!!

Maswali yamekuwa ni rafiki wa akili na hasa katika kupasha joto ubongo, na upelekea hali nzuri kwa akili kupanuka na kupata uelewa mwingine.

Na wakati mwingine mtu anapokosa jibu hali hiyo uweza kuingia ndani ya moyo na kuleta usumbufu, usumbufu wa mtu kuwa na maswali mengi kwa kile kinacho mkabili pasipo kujua niende kushoto au kulia, hali ya swali kuwa na jibu zaidi ya moja na hatimaye kushindwa kupata jibu linalojitosheleza na hata kujikuta uko njia panda.

Pindi inapotokea mtu anapokuwa na maswali mengi kichwani mwake kwa kiasi kikubwa inategemea hulka ya mtu husika wako watu wanapokuwa katika hali hii upenda kucheza mziki, au kupiga makelele,kuongea sana, kukaa kimya na mwingine upenda kulala hama kulewa na mambo mengine yafananayo na hayo lakini bado unaweza kukosa jibu sahihi au lililojitosheleza katika swali husika.

SWALI LINAKOSA MAANA PALE UNAPOPATA JIBU!

Kama samaki anapo poteza makeke yake au usumbufu wake ni pale utakapo fanikiwa kumtoa nje ya maji na kumweka nchi kavu………………………………………………..!

Ndivyo ilivyo pindi utakapopata majibu katika maswali yanayo kukabili hapo akili uweza kutulia na hali ya ushwari uweza kuingia ndani ya moyo wako.

Ndomana waswahili usema “ atafutae achoki na akichoka amepata” hivyo utashangaa pindi mtu atakapo choka wakati ajapata japo yote yanawezekana kutegemea na hali ya ndani ya mtu husika .

Na wakati mwingine unaweza pata majibu lakini sio utatuzi wa leo wala kesho bali utakuweka katika hali njema ya matarajio ya uhakika wa kweli katika majira yajayo.

Usiruhusu maswali yawe maisha yako maana yatautesa ufahamu wako! Bali tambua kwa kila jambo/swali linalokuja katika maisha yako uwa tatizo linaisha ni mpaka ujue majibu ya maswali hayo yanapatikana wapi? Maana ukikosa kujua sehemu husika hauwezi pata majibu ya uhakika.

“ hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea”

1 Wakorintho 10:13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.

Endapo ikatokea ukakosa majibu ya maswali yako kwa wanadamu ( watu unao waamini) usihofu wewe fungua hazina ya mbingu hiyo uwa haikosi majibu maadam mbingu hipo basi mwenye mbingu yupo na majibu yapo.

Haya ni majibu yanayoleta amani ya kudumu, maana hicho ndicho chanzo sahihi cha majibu ya maswali yako.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………………0764 018535

Ijumaa, 20 Julai 2018

CHA MUHIMU KWANGU!





“ ukristo wangu ndio maisha yangu”

Uzuri wa dunia na utamu wake ni kwamba kila mtu anakitu kwake anakiona kuwa ni muhimu kwake, lakini tatizo linakuja pale tu kitu kimoja kila mmoja akakiona ni muhimu kwake na kutaka kuwa nacho kwa muda mmoja hapo ugomvi na chuki uweza kuzaliwa.

Kama binadamu kuwa na kitu cha muhimu ni jambo la kawaida, kwa kuwa kila binadamu ana mwelekeo wake hivyo upelekea hali ya mtu kuwa na kipaumbele chake, japo anaweza asijue kuwa jambo hilo kipaumbele kwake ila hicho kitu kitachukua nafasi kubwa katika moyo wake na hata hisia zake.

Japo umuhimu wa kitu (kipaumbele) ubadilika kulingana na mazingira husika na hali iliyotokea mathalani baba anaweza kuweka kipaumbele kwa mwanae lakini inapotokea mwenendo wa huyo mtoto kutoufurahisha moyo wa baba, hivyo umuhimu wake unaweza kushuka na hatimaye kipaumbele kubadilishwa.

Cha Muhimu kwangu! Ni hali ya mtu kuwa na kitu kitakacho kukuwezesha kuwa katika hali yako ya ubora na ustawi na kwa umakini wa kufuata maelekezo kwa uangalifu wa rohoni na mwilini.
Ndomana unaweza usishangae kwa kipindi cha kwanza mtu anaweza fanya kitu kilicho bora au kizuri lakini pindi unapopoteza umakini katika kipaumbele chake ( jambo la msingi katika kufanikiwa kwake) basi hapo unawezafanya kitu kilekile na kwa namna ile ile lakini matokeo yakawa tofauti na alivyotegemea. 

Kuna wakati unaona kuna mambo mengi ya kufanya ukashindwa kuchukua hatua au kufanya maamuzi sahihi katika kutoa nafasi ya kwanza kwa kile kitu muhimu au kilicho kuwezesha kuwa pale.

Unaweza kukuta mtu alikuwa na huduma ilipoanza kutumika ikaleta matokeo mazuri na hatimaye kupelekea kufahamika na kuzidi kugusa maisha ya watu wengi na katika hali hiyo ukajikuta kupenda sifa na kutopenda kushuka ( kama ilivyo asili ya Mungu ndani ya mwanadamu) na hata kuanza kupelekwa na kila upepo kushoto au kulia na hatimaye kupoteza chanzo cha ubora/ ustawi wake.

Sio mara zote msingi wako ( chanzo cha ustawi) unapo poteza ukajikuta uko chini, unaweza kupoteza chanzo cha ustawi wako lakini ukakuta hakuna mabadiliko ya inje yanayoweza kukutisha hivyo ukaendelea na msimamo wako pasipo kujali mng’ao wa kesho yako.

Lakini dalili kuu ya kutambua kuwa chanzo chako kilichopelekea mng’ao wako kimepotea ni ongezeko la tabia za mwilini.( ubinafsi na kujiami zinakuwa na nguvu sana kwako ).

Kwa Yule ambaye ajapoteza chanzo japo upepo na dhoruba zinaweza kumsonga lakini hali ya uhakika wa kesho yake iliyojaa amani na tumaini la mbingu linakaa ndani yake.

Ni muhimu kuwa makini na utendaji wa mbingu katika maisha yako ( huduma/ shughuli unayoifanya).

Na mtu wa namna hii ( anayetambua chanzo na kukithamini ) uwa hana mashindano bali usimamia kwa ufasaha wajibu wake.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………0764 018535

Ijumaa, 29 Juni 2018

KIVUTIO CHA MUNGU!




MUNGU ANGALII UNA NINI ILI APAE NAWE BALI KIASI GANI UMEMJAA YEYE HICHO NDICHO KIVUTIO KWAKO!

Moja ya kitu kinachoangaliwa na watu wengi ni muonekano na sio mbaya kwani hata Mungu ujali sana muonekano wako hasa wa ndani maana ndio wenye tija kwake.

Maana muonekano wa ndani ndio wenye kubeba  uweza mkubwa wa kuitawala tabia yako ili uweze kutimiza kusudi lake Mungu ndani ya maisha yako.

Ni kweli ukiwa na mali hicho kinaweza kuwa ni kivutio cha watu wengi kwako, jina lako linaweza kutajwa kila mahali hata pale ambapo ukutarajia si kwasababu vile ulivyo bali kile ulichonacho.
Utofauti mkubwa uliopo kati ya binadamu na Mungu ni namna anavyoangalia mambo…………………………!

1 samweli 16:6 Ikawa walipokuja, alimtazama Eliabu, akasema, Yakini masihi wa BWANA yupo hapa mbele zake.

 7 Lakini Bwana akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo.

“ mimi siangalii kama binadamu wanavyoangalia”- Mungu!

Kwa kuwa jicho la Mungu linaona hitimisho lako, kwa kila tendo unalolifanya linaweza kung’arisha hitimisho / hatma yako au kuiharibu.

Moja kati ya vitu ambavyo Mungu atingishwi nacho ni mali ulizonazo  ( wealth ) japo mali ulizonazo zinaweza kuwa tishio kwa watu na hata kuwavutia wengi kwako na inaweza hata kupelekea hata kubadilisha jumbe za wachungaji/ wahubiri ili mradi tu wewe uendelee kuwepo kanisani lakini sio Mungu.

Ibrahimu na Mungu!

Mwanzo 22:9 Wakafika mahali pale alipoambiwa na Mungu, Ibrahimu akajenga madhabahu huko, akaziweka tayari kuni, kisha akamfunga Isaka mwanawe, akamweka juu ya madhabahu, juu ya zile kuni.

 10 Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe.

 11 Ndipo malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akasema, Ibrahimu! Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.

 12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.

“ kama ukuweza kumzuilia mwanao wa pekee isaka hakika kukubariki nitakubariki “
Mungu sio apendi tuwe na mali ila mali bila yeye ni maangamizo maana mali inaweza kukuendesha na hata kupelekea maafa yako.

Tatizo sio kupata vitu! Kwani mtu anaweza kuwa na pesa matumizi yake yakakosa mafuta, tunajua kazi ya mafuta ni kufanya kitu kwenda pasipo ukakasi au kulazimisha kwa ugumu ndivyo mtu anaweza kuwa na pesa lakini akawa anatumia vitu avielewi mara hili au lile mambo yanatokea mengi mara huyu mgonjwa au ajali yaani mambo yamepangana tu yote yanakula hela tu mpaka zinakwisha.

Lakini hela zinazoambatana na mafuta ya Mungu zinatumika lakini haziishi sawa na yale mwanamke mjane aliyekuwa na kibaba cha unga anachota haviishi.

Kivutio cha Mungu ni moyo uliye mjaa yeye usiobadilishwa na upepo hama kushawishika na mali maana sio changamoto kwake, maana pindi utakubali kuwa chini ya himaya yake basi kukutunza ni jukumu lake.

Kwahiyo unapoenda kwa Mungu ujue hakuna kitu kitakacho mvutia kwako zaidi ya moyo uliomjaa yeye.

“ Mtu huyu ndiye nitakaye mwangalia mtu aliye mnyenyekevu, mwenye roho iliyopondeka……”

Isaya 66:2(b)….lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………….0764 018535


Ijumaa, 27 Aprili 2018

MUNGU HAONGWI




Moja ya kitu kinachoweza kukuonyesha kuwa wewe ni wakisasa ni uwezo mkubwa wa kupata fursa pasipo kujali hizo fursa unazipataje? ( unatoa rushwa au hautoi ).

Imekuwa ni mtindo wa kisasa na kukubalika kwa haraka kama sio kwa wepesi katika jamii kwa kundi la watu fulani, vitu vingi ili uvipate utahitaji lazima ulainishe viwe rahisi kuvipata au kuvimeza, ndomana kukaibuka na misemo mingi iliyo na maana iliyo wazi au imejificha kama vile, ili ule lazima nawe uliwe, mtaka cha uvunguni sharti ainame, ukitaka……………..penyeza rupia, ukipenda boga  penda na ua lake na misemo mingi yote ni katika kujirahisishia ili mambo yako yaende.

Imekuwa ni kawaida kana kwamba ni mafuta kwenye gari kwakuwa gari aliwezi kwenda pasipo mafuta ndivyo imekuwa bila ya kuongwa au kuonga maisha hayaendi sawa, hivyo ndomana mtu akitaka kitu/mtu ( msichana au mvulana ) lazima aonge kama njia ya rahisi ya kupata uhitaji wake sio hilo tu hata mtu akitaka kazi anaweza kuweka uwezekano wa kutoa ongo na hii imeenda mbali kidogo hata unapotaka ( haki yako ) utoshangaa mtu akitoa ongo au kudai/akitaka ongo.

Imekuwa kwenye akili ya watu kiasi kwamba mtu akipata huduma/ kitu pasipo kutoa ongo uweza kupata wasiwasi na kujiuliza hii hali/jambo linawezekana vipi? Kwa hiyo anapotoa hivyo uweza kujisikia vizuri na kupata uhakika zaidi kuwa hicho kitu atakipata au ni chake.

Hali hii imetawala na kuzidi mpaka inatisha na kuonekana ni kitu cha kawaida na kufanya rangi nyeusi kuonekana nyeupe, kitu ambacho si halali sasa kimehalalishwa.

Naam hali hii imefunika macho ya watu mpaka kuona mtindo huu unaweza kutumiwa hata kwa Mungu.
Pindi mtu anapokuwa na shida au uhitaji unaenda na kitu kwa Mungu, ukitazamia jicho la Mungu likuone huruma na kunyosha mambo yako na hivyo hali hii imepelekea hata watumishi kushawishiwa na kuona njia rahisi ya kuwapata watu na fedha ni kubuni utaratibu fulani kwa kuwatoza hela kwa kila tatizo na ukubwa wa tatizo ndio wingi wa hela na kushawishi hata kusema ili utoke kwenye shida/tabu yako ni lazima utoe kitu.

Sauli “ bwana upendezwa na dhabiu kuliko kuitii sauti ya bwana”

I samweli 15:22 Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu.

Ni muhimu kutambua sio utaratibu wa Mungu kuwa lazima utoe pesa ili upokee bali anataka maisha yako kwa ujumla umpe yeye…………………..japo na kubaliana kabisa Roho mt. anaweza kukugusa utoe kitu ili uweze kutoka katika shida/maangamizi yako.

Hii hali ya kutoa ili upokee pasipo kujua unapokea unatakiwa kupokea nini? Hali hii ni hatari sana katika maisha yako na Mungu, kwa maana usipoiona au kupata vile ulivyotegemea kuacha wokovu ni jambo linaloweza kutokea wakati wowote.

Ni muhimu uhitaji wako kwa Mungu ujengwe katika PENZI ( itokee au isitokee ) isikupe shida ili mradi penzi lipo usiwe na hofu ustawi utakuwepo tu.

Usipende sana kuwa makini katika kuona uhitaji wako unatatuliwa bali elekeza umakini wako katika penzi lenu linakuwa siku kwa siku.

Ndani ya penzi kuna kukidhi mahitaji yenu pasipo msukumo wa nje yenu ( kila mmoja uwajibika kwa ajili ya mwenzake ) wala hakuna kutegemeana/ kutegeana.

Kunatofauti kubwa kati ya kuomba kukidhi uhitaji wako ukiwa ndani ya penzi na inje ya penzi.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………….. 0764 018535