Jumanne, 28 Juni 2016

ASANTE KWA HILI...............!!!



ASANTE KWA HILI

Naweza sema ni neno tamu na lenye mvuto wa kipekee na hasa kwa mtu uliyetegemea aseme ASANTE! Naye akakubaliana na sauti ya moyo wako na hatimae akasema ASANTE! Na amini utaona kama unaota na hatimae moyo wako utakuwa na furaha itakayokosa kificho katika muonekano wanje!

Na kubaliana kuwa neno ASANTE linafuata baada ya tendo jema mtu alilotendewa, japo kuna wakati unaweza kutendewa jambo jema lenye maana baadae ila pasipo kujua ni jambo jema kwako unakosa kuwa na moyo wa shukrani kwa wakati huo……….mathalani mwanafunzi anapoaandaliwa kuwa mtu fulani katika jamii yake hasa kutokana na kipawa chake bila shaka katika matengenezo ya kuwa mtu bora sio rahisi kusema ASANTE.

Changamoto kubwa katika kushukuru kwa jambo unalotendewa ni wazi inakuwa vile watu wote hamjui mnalopaswa kufanya kwa kuwa inakuwa ni mission ya Mungu katika kumwandaa mtu kuwa MTU hivyo mnakuta huyu ampendi huyu na huyu anamchukia huyu kumbe hiyo hali inasababishwa na jambo linaendelea ndani ya Mungu ila hapo kunakuwa na udhihirishi tu.

Niseme kuna siri kubwa sana katika kusema asante (shukrani) kuna minyororo inavunjika, kuna kuta zinabomoka na thamani yake kamwe huwezi kulinganisha na chochote kwani liko vile kama lilivyo hakika hili neno limebeba utoshelevu na mbaraka wake usio kuwa wa kawaida ni wewe kuutambua tu.

Nimeona mtu akikatisha kumsaidia mtu kisa kilikuwa huyu mtu ajui neno ASANTE kinywani mwake hivyo haoni kile ninachokifanya kama ni cha maana katika maisha yake hivyo sijisikii kuendelea kumsaidia maana yeye haoni jinsi ninavyojinyima juu yake hivyo ni bora niangalie kitu kingine ambako Moyo wangu unasukumwa kuwa huko.

Katika yote ni bora uone hivyo katika upande wa wanadamu wenzako kuwa awanashukrani lakini wanadamu sasa hivi imekwenda mbali sana kiasi cha kuona hata Mungu pia amewekwa katika kuchunguzwa kana kwamba ni binadamu kwani nini anitendei mimi au haoni juhudi zangu kwa ajili yake! Watu wamekuwa na kisasi sio kwa wanadamu bali wamevuka mpaka hata kwa upande wa Mungu kana kwamba na yeye walishirikiana hama kushauriana ili kwamba yeye atokee dunia na kujichagulia maisha hayatakayo na sio aliopangiwa kuishi.

ASANTE KWA HILI……….usipo ona kuwa Mungu mwema kwa yale yana yofanyika yaliyo nje ya uwezo wako basi hakuna jambo ukampa thamani yako Mungu katika hali stahiki na katika mwendelezo unaotakiwa!

Imekuwa kama mtu ukamfanyia mema mengi pindi anapoona pungufu lake moja basi uweza kusahau yote basi linakuwa na nguvu zaidi ya mema yake yote , hivi ndivyo watu wanavyoona kwa Mungu laiti ukikaa chini na kutafakari na kuona jinsi Mungu alivyo mwema katika maisha yako kamwe usinge fungua mlango mwingine wa kuona upendeleo wa Mungu kwa wengine kuliko kwako.
Samahi kwa mfano huu japo sio wote, usiwe na hasira kama mama mjamzito katika miezi ya awali kwani unaweza ukamfurahisha katika mambo mengi ukimuuzi kitu kimoja tu basi anaweza akasusa na kuona kila kitu kibaya kwake.

Lazima ujifunze kuona pamoja na yote lakini katika hili Mungu ni mwema sana  ASANTE KWA HILI kwa kuwa hakuna kipimo cha kupima wema Mungu katika maisha yako na laiti pangekuwa na mizani kati ya Mungu kwa yale apasayo kukutendea na kwako kwa yale upasayo kutenda kwake kamwe pasingekuwa na hata kushamiliana hata chembe na amini utajiona kuwa wewe ni mkosaji sana japo Mungu haoni yale unayo yawaza  na kujihukimu basi upaswi kuona kuwa Mungu sio mwema kwako.

Ni vizuri utambue unapo mzungumzia MUNGU sio kitu fulani ambacho unaweza ukakiweka unavyotaka nacho kikawa kwa namna unavyofikiria, ni vizuri utambue kwa sababu yake ndomana wewe uko japo upaswi kumuogopa zaidi sana PENZI lake likuongoze naamini utakuwa salama.
Jifunze kumshukuru Mungu hata kwa madogo maana ndio mapenzi ya Mungu kwetu, maana Mungu yeye ndie awezae kuamuru jambo jema kukufuata popote ulipo pasipo kuangalia umbali gani uliopo kati yako na mbaraka wako.

Usiruhusu kufikia maamuzi ya kuona Mungu ameniacha sasa naweza fanya chochote tambua sio kila mawazo yanayokuja kwako yamebeba usahihi hivyo usiruhusu kuwa hayo ndio maisha yako ya kuona Mungu ahusiki katika maisha yako.

Ni kweli mawazo mazuri ni kitu kimoja lakini bila neema yake uwezi kukamilisha tambua upana wa Mungu na Upendo katika kila hali inayokuzunguka na hapo ndipo uone NJIA YA KUTOKA!! NA SIO  LAWAMA,

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………0764 018535

FURAHA YA MUNGU IWE NCUVU YAKO

Jumanne, 21 Juni 2016

INAITWA KESHO



INAITWA KESHO



Ki ukweli sina jina jingine zaidi ya kusema kuwa inaitwa KESHO! 

Na swali kwako ni kweli unaipenda kesho? Na unaweza kutofautisha mtu anayeichukia kesho yake na anayeipenda kesho yake? Karibu………………..!

Ni siku baada ya leo au kwa jina jingine uweza kuitwa ni masaa 24 yajayo, unaweza usiipende sana au ukaipenda lakini bado itabaki kuitwa KESHO na bila shaka kama Mungu akikujalia NEEMA ZAKE basi utaiona! Wapo waliona kesho kama ni siku tu ya kawaida hatimae ilipofika walijuta hivi kwa nini KESHO imekuwa LEO na bila kusahau wapo walioiogopa sana KESHO naam pindi ilipofika walipata raha sana na hata kujiuliza hivi kwa nini nilikuwa naiogopa sana kesho. 

Imekuwa kauli ya kawaida sana ikisema bora mtu akucheke LEO kuliko akucheke KESHO! Kwa maana rahisi wacha acheke LEO ili KESHO akuheshimu itakuwa picha nzuri na bila shaka italeta picha nzuri na kutambua yupi wako na yupi umesingiwa tu ila ki ukweli akuwa wako.

Bila shaka KESHO inaweza kuwa majibu ya wengi na utatuzi wa wengi katika maswali yao na wengine kuwa chanzo cha furaha na upendo miongoni mwao! Imekuwa jambo la kawaida sana kutaka kujua kitu kilichobora watu watasema kisifae kwa LEO tu bali hakikisha kitatumika hata KESHO.

Ni jambo la kawaida sana mtu kusema kuwa maana lazima awe tayari kwa LEO na hata KESHO yaani akufae leo na hata kesho maana kama umepewa kuiona pamoja naye basi utaitaji utumie vizuri pamoja nae kama Mungu akiwakupa neema kuiona.

Sikatai binadamu yeyote mwenye akili timamu bila shaka atakuwa anajitahidi sana kuiweka kesho kuwa na picha nzuri na pindi itakapofika basi ajisikie fahari zaidi ya LEO na kuona alikuwa anastahili kuwa hapo na mahala hapo palistahili yeye kuwepo na kamwe apamchoshi zaidi ya kupafurahia tu.

Japo sipingani sana kusema usiifurahie Leo ila napenda kusema pindi utakapoamua kuifurahia leo bila shaka weka mazingira mazuri ya furaha yako kuwa kuu KESHO kwa maana LEO yako hasa ujengwa na KESHO sio leo kwakua Leo itapita ila KESHO utafika……….kwa hiyo kuipenda sana njia kuliko mahali unapo pumzika ni hatari  kwa furaha endelevu.

Ki ukweli baadhi ya mambo ungelikuwa una angalia KESHO yake usingetia bidii kuyafanya sasa ila kwakua ujui kesho yake kwa ufasaha zaidi hivyo unaweza kujikuta unajikita zaidi sana kuibomoa kesho yako kwa kuipenda LEO yako.

Sina tatizo kwa wewe kuipenda leo ila ninatatizo la wewe kuipenda leo kuliko kesho yako! Japo na amini sababu moja wapo ya kuipenda leo kuliko kesho ni vile leo unaiona na kesho hauioni hivyo unaweka bidii kwa kile unachokiona pasipo hatari zaidi ya kile usichokiona na pindi kitakapo kufikia kitakukuta katika hali gani? Sina jibu.

Ni vizuri unapoiangalia LEO basi iangalie sana kwa umakini sana KESHO kwani katika hilo kunaweka usalama mkubwa wa kesho yako…..na utakubaliana nami kwa hili wale wengi walioijari kesho yao zaidi leo kwa jina lingine wanaitwa wawekezaji walijisikia vizuri pindi kesho ilipofika maana walifanya kwa ajili ya siku inayofuata na sio kuitengeneza JANA yao ili leo yao iwe na muonekano mzuri.

Ni vizuri kutambua tu kuwa haijarishi uko wapi au unafanya nini au unaweza nini au unatamani nini katika yote bado kesho itafika na itakuwa sawa na kanuni yake! Kwani hauwezi kupanda mkorosho ukategemea kuvuna karanga hapo hapaitaji imani wala busara yoyote bali kanuni inavyosema ndivyo itakavyotokea.

Niseme wazi ni bora uchoke leo maana inaweza ikatengenezeka kuliko kuchoka kesho pasipo kujua utakuwa katika hali gani? Na msaada gani utaupata na je! Uo msaada utakuwa wa maana kwako itategemea sana na namna itakavyo kukusaidia au kukubomoa kabisa.

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson………………………………………………….0764 018535

Jumanne, 14 Juni 2016

UNAMUONA NANI?



JIONE MWENYEWE!


Kioo kimekuwa kitu kinachotoa hukumu kwa watu wengi kama sio wote, wapo watu baada ya kujiangalia kwenye kioo wanajikubali sana na wapo watu  wanaojiangalia kwenye kioo na kuona bado kuna mapungufu katika muonekano wao na kundi lingine pindi linapojiona katika kioo wanajichukia ghafla na bila kusahau marafiki zangu wengine pindi wanajiangalia kwenye kioo wanakuwa na hali ya kujikataa kabisa! Sijajua upande wako?
 
Lakini katika yote tunaona moja ya kazi ya kioo ni kutoa taswira yako lakini watu wengi wangependa  kingepewa uwezo kuwatengeneza na kuwa sawa na fikra zao wakati huo zinavyopenda maana kila kipindi kunakuwa na mabadiliko katika kutimiza matamanio fulani.

Moja ya kitu ambacho kina wa kwamisha watu wasifike mbali na kuwa vile wanavyopaswa kuwa kwakua wamejikataa wenyewe binafsi na kuanza kuishi katika hatua za wengine…. japo unaweza usione shida kwa kuwa wewe binafsi umeshapenda mtindo wa kuishi kutokana na kuona mtu akienenda katika njia fulani na mbaya sana ikitokea amefanikiwa katika kiwango fulani basi wewe ukaona njia yake ndio njia yangu.

Mtu yeyote unaye muona kuwa yuko juu unaweza usijue mtu huyu mpaka kafika hapa ametengenezwa vipi au na nani? Na pengine huo mng’ao wake unao uona ujui msingi wake hasa nini hasa kimemweka hapo! lakini ndugu yangu umezama na kuishi maisha ya mtu mwingine kujiamini na kuona hivyo ndivyo unatakiwa kuishi.

Niseme tu ni vigumu sana kufanikiwa kwa kupitia nyayo za mwenzako ukiamini kwakua yeye kafanikiwa basi bila shaka nami nitafanikiwa pasipo kujua ili mtu afanikiwe kuna vitu vingi vinausishwa na bila shaka kuna vile anavyovijua muhusika na vingine havijui ila vina kuwa na mchango katika kumfanya mtu maalum katika jamii yake.

Niseme tu hakuna kitu kizuri kama kujiona wewe mwenyewe katika mwenendo mzima wa maisha yako kwani kinakupa kujiamini na kujisikia vizuri na wala upotezi muda kutafuta mtindo nje yako bali utumia muda kuvumbua vitu vilivyo katika maisha yako na vinakuwa na radha yako hivyo watu wa kikuona wewe wana ona namna yako katika mwenendo wako.

Sikatai kitu kinacho wafanya watu wengi wasiwe wenyewe moja ni haraka katika kufanikiwa wana amini sana kwakua mwenzangu alitumia njia hii na kufanikiwa basi hakuna shida hata mimi nikitumia njia hii ya mwenzangu nitafanikiwa pasipo kujiweka katika namna yako utachukua  muda mrefu ili kufikia mahali ambapo mwenzako amefikia.

Sikatai kujifunza kwa wengine katika mambo yao katika ujumla wa mwenendo wao wa kufikia hatima yako lakini sio kuchukua maisha yao na kuanza kuishi kwa namna yao na ukijisahau kuwa wewe ni siri ambayo inahitaji wakati, mahali sahihi ili ijifunue na hatimae nawe uweze kujishangaa kama wewe unavyo washangaa wengine.

Ni vizuri utambue mtu yeyote unaye muona yuko katika mng’ao fulani jua alianza moja au alikuwa na mwanzao wake ambao kama ungeliangalia mwanzo wake usingeweza kuamini kuwa leo atakuwa vile unavyomuona……..kwani mabadiliko yakifika lazima yambadilishe katika mng’ao na sio lazima abadilishe ngozi yake bali ni katika kunawiri na kujiamini zaidi.

Ni ukweli usiopingika Mungu anapenda uwe vile alivyokuumba kwani yeye ndiye alikutengeneza na bila shaka analokusudi la wewe kukuweka katika namna/hali hiyo hivyo unavyojikataa bila shaka unataka kumrekebisha muumba wako na kuona yeye alikosea kukuweka katika mwenekano.

Niseme usiogope mwanzo utaanzaji bali ningekushauri uogope sana mwisho wenye kukudhihirisha wewe kuwa ni nani ambao utabaki kama ushuhuda katika maisha yako na katika jamii yako.

Usiogope kuchukua maamuzi hata kama ni magumu sana ili mradi yamebeba manufaa katika kesho yako ya chukue tu watu watakuelewa baada ya kuona yamekuwa vizuri.

Utofauti ambao Mungu ameuweka katika dunia ya sasa ni vizuri ungeheshimiwa ili hile picha yake ikamilike maana yeye akukuumba kimakosa na wala ahitaji kukosolewa kwa maana hata wewe ukujua kama utakuwepo ila yeye alijua basi heshimu maamuzi yake, na penda kufananisha hali hii ni kama mwili wa binadamu ukiwa na viungo vingi na kila kiungo kina kazi yake na kina namna yake japo inawezekana lakini sio vizuri kazi ya mikono ikafanya na miguu hasa kwa mwanadamu aliye kamili kila kiungo kiliumbwa kwa kazi yake.

Niseme vyovyote ulivyo wewe ni bora, unaweza , unatosha sana! Na hakuna mbadala wako!

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………………………..0764 018535

NIKISEMA SIKU NJEMA NITAKUWA SIJAKOSEA!

Jumanne, 7 Juni 2016

NAJUAJE KAMA NAMJUA MUNGU?



NAJUAJE KAMA NAMJUA MUNGU?


 Katika maswali ambayo watu wengi hawatafikiria sana ilikutoa jibu, ni swali hili JE! UNAMJUA MUNGU? Watu wengi watasema yah! Kwakua naenda kanisani, nasaidia watu, naishi vizuri na majirani zangu, nina biblia nyumbani, na wengine watasema uwa wakati mwingine nikipata nafasi kutokana na majukumu yangu naenda kanisani kwakua natambua yeye ni muweza wa yote, na wengine wataenda mbali kidogo wanasema mimi mchungaji wangu ananijua na ameniambia nitakuwa mtumishi mkubwa kwakua ndani yangu ameona huduma kubwa na hata mtaani kwangu watu wananihita mchungaji! Na wengine watasema mimi hata mapepo yananitambua na yana niogopa na mara mtu mwenye mapepo anaponiona uwa anapiga kelele yaani ni kama yesu anapokutana na mtu mwenye pepo! Uku ndiko kumjua Mungu swali jepesi?

Ukweli watu wengi tumekuwa tukijifunika sana katika kutembea katika vipawa tukiamini katika hali hiyo basi sisi tunamjua Mungu sana hata kuliko watu wengine ambao hawatembei katika vipawa vyao! Hivyo nasi ikatupelekea kujihesabia haki au kujipa nafasi ambayo tuna amni kuwa tunastahili kuwa nayo kwa hiyo tunaweza kuwanyoshea vidole wengine kuwa Yule bado sana! Mpaka anifikie mimi sijui mpaka lini labda mwaka 3000 Mungu akitujalia.

Niseme wazi ili jambo linajibiwa vizuri hata mtu asiye okoka pindi utakapo muuliza kuwa wewe unamjua Mungu atasema pasipo shaka anamjua ten asana mbali zaidi uwakute wasomi wenye uelewa mdogo kuhusu Mungu wanaweza kushusha data mapaka ukasema hakuna asiye mjua Mungu katika ulimwengu wa sasa, hata kama anajua wakati mwingine anakosea uweza kusema japo najua ninachofanya ni makosa lakini najua usahihi ni upi kwa maana namjua Mungu japo na mkosea sana lakini na amini siku moja atanisaidia tu ni taka vizuri sawa ninavyojua.

KUMJUA MUNGU! Kumekuwa ni jambo la kawaida sana kwa kuwa kila mtu anasema anamjua Mungu kwakua asilimia kubwa ya wanadamu wana amini Mungu yupo japo wako watu ambao wanaamini hakuna Mungu katika dunia ya sasa bali ujikita zaidi kwenye sayansi na teknolojia pamoja na uvumbuzi wa mambo mbalimbali yenye kuwapa kiburi na majivuno kuwa wao wanaijua dunia kuliko hata mwenye dunia.

Mbaya zaidi hata watu waliokoka wanaaminika kuwa wanamjua Mungu na kuwa kielelezo safi katika kuwaonyesha jamii kuwa mtu anayemjua Mungu anatakiwa aweje! Lakini wamekuwa wakipeperushwa uku na kule na kutoa ushuhuda mbovu kwa watu wasio okoka wanaoenda kanisani wengi wamekuwa wakiwa waongo sana katika mambo mengi mathalani kuomba kazi, mausiano, kujirahisisha na wakati mwingine kushiriki katika vitendo vya kuwadhulumu watu, rushwa na mengine mengi kwa namna hiyo imekuwa ni kawaida kwa mtu asiyeokoka kuamini anamjua  Mungu kama kuokoka namna hii basin a yeye anamjua Mungu na hali hii imekuwa ngumu sana katika kuwatofautisha watu waliookoka na wasiokoka! Lakini jambo alimtishi kwa mtu ambaye ameamua KUMPENDA MUNGU KWELI.

Nipende kusema kuwa KUMJUA MUNGU sio kitu kidogo na wala sio kitu kigumu sana kipo na kinawezekana tu endapo utakapoamua kwa dhati kuwa sasa nataka kumjua Mungu. Kwani katika kumjua Mungu ndivyo unaweza kukaa naye katika ubora na kumtumikia kwa uhuru zaidi pasipo mashaka yoyote.

Na mtu anaye mjua Mungu kamwe hawezi kujiona kuwa amefika kiasi kwamba Mungu amekuwa shemeji yake hivyo anaweza kumtania anavyotaka kana kwamba ameenda kule aliko Mungu na hatimae amerudi kutusalimia tu!

Kumjua Mungu ni kitu kingine na mtu anaye mjua Mungu ni kitu kingine anaweza kumdhihirisha Mungu kwa uhalisia na watu wote wakamuona pasipo shaka na wakaelewa na kukubali kuwa huyu ni Mungu mwenyewe wala hakuna udanganyifu wowote.

Sio swala lakusema mimi na mjua Mungu kama kusema hata viumbe wengine wanaweza sema tena vizuri haijarishi wanaelewa au awaelewi!

Kuna kuanza KUMJUA MUNGU na kuendelea KUMJUA MUNGU! 

Yote inakutegemea wewe binafsi unavyoenenda na Mungu na sio namna unavyoenenda na rafiki, mchungaji wako.

NAJUAJE NA MJUA MUNGU!

I.Mtazamo wa Mungu katika maisha yako.

Ni kweli maisha yako ni bora kuliko Mungu au Mungu ni bora kuliko maisha yako!
Ukitazama maisha yako kama kioo ni kweli unaona thamani ya Mungu katika maisha yako. Unapoona maisha yako ni kweli unaona nafasi ya Mungu katika kunawiri au kuwa mshindi katika maisha yako. Ni kweli moyo wako unaona uzuri wa Mungu, upendo wa Mungu ukidhihirika katika maisha yako?

Ni namna unavyomuona bila shaka ndivyo utakavyoishi maisha pamoja na Mungu au mbali na Mungu ahijarishi unaenda kanisani au ahuendi kanisani!
Nidhamu yako mbele za Mungu ndio itakupa mwenendo wako na Mungu katika uharibifu au katika ustawi.

Maisha (ni mwenendo binafsi unavyoenenda kila siku) sio familia bali ni namna unavyo muona Mungu alivyo wa muhimu katika maisha yako ni vile unaona pasipo msaada wa Mungu ni ngumu kutoka pale ulipo ni ngumu kuwa salama pasipo yeye kuhusika na maisha yako.
Wako watu wanaona bila kitu Fulani maisha yao ni taabani mathalani bila mchumba,kazi,rafiki maisha yangu hayaenda inavyotakiwa .

II.Mtazamo wako juu ya changamoto zako.

Matumaini ya moyo wako yanapo didimia ni kweli roho yako ina nguvu ya kusimamisha na kuendelea kumwamini katika NJIA SAHIHI.

Hapa ndipo unaweza kuona maajabu unaweza kukuta mtu anabiblia alafu ana hirizi, hivyo akienda kanisani anabiblia na akirudi nyumbani anaiamini hirizi au kingine chochote mbadala wa Mungu.
Mbali na hilo unaweza kukuta mtu aliyekuwa na imani nzuri yenye utisho ukakuta amekuwa katika imani isiyo sahihi kabisa nay eye uko amezama sana.

Ukisikia kiini cha mwanadamu kutoka kujidhihirisha ana amini nini aua anajua nini ni hapa katika kiti moto kitakachomfanya awaze kukaa lakini aone uwezekano wa kukaa kuwa imeshindikana, akasikia hali ya kukimbia lakini akakuta anashindwa kukimbia kwa kufupi lile analowaza sio lile analolitenda.

Changamoto zipo kwa ajili ya kuinua uende katika daraja linguine na inapokuwa shida kwako kufaulu kwenda katika daraja linguine ndipo hapo unaweza kuchukua muda mrefu katika hatua Fulani pasipo kupata.

Kumjua Mungu ni namna Mungu anavyozifunua siri zake! Ili uimarike zaidi.

Imeandaliwa na;
Cothey Nelson……………………………………..0764 018535