Jumanne, 19 Mei 2015

UPEPO UNANIPOTEZA



UPEPO UNANIPOTEZA


Upepo ni kitu chema sana na ni kitu kizuri kwani ndani yake hakuna ubaya uliobebwa ndani yake , tangu ulipoamliwa kuwepo haukubeba ubaya wowote….. wala muumbaji wa huo upepo hakuwa na kusudi baya ndani yake……..japo inategemea uko upande gani katika wepesi au uzito stahili kwani upepo umekuwa kero kwa wengine na wengine kuwa kiburudisho mathalani kwa wale walioanika nguo upepo una uzuri wake lakini kama ikitokea una nguvu unaweza kukuta nguo mahali zilipo hazipo tena ikawa huzuni badala ya kufurahia hewa safi inayopatika!!

Ninapozungumzia UPEPO hapa na zungumzia hali ya wakati na kukubaliana na huo wakati ni kama vile nguo zinaposhindwa kuimiri kishindo chake basi uondoka sawasawa na upepo unapotaka kwenda pasipo kujali ulikuwa tayari au sio kwa utayari!!

Na ninapo zungumzia UPEPO na zungumzia mambo  mbalimbali yanaendelea katika dunia yaliyojaa mapinduzi mengi na hata kufanya yaliyo halali kufanya sio ya halali na hata kinyume chake ni kama vile upepo umekusanya mambo mengi sana…… vitu vingi vinabebwa na upepo alafu vinaachwa pasipo kurudi tena katika hali yake ya awali lakini pindi nguvu inayo kuja pale wakati inakung’oa utafikiri haitakuacha lakini inakuacha pasipo kujali utaendeleaje au utaponaje! Katikati pasipo muelekeo laiti ungeuona mwisho kabla ya mwanzo usingekubaliana kwenda na nguvu zake.

Lakini sasa mambo yanayo endelea katika dunia ni kama upepo yanakuchukua kwa nguvu na kukuacha mahali ambapo uweza kwendelea na hata kujua kama utakuwa hapo ndomana katika mwisho katika mambo ya kidunia mwisho wake tunaona vijana wakijingiza maisha yasiyo na mfumo maalum na mwisho ujikuta wamepata magonjwa ambayo ni pigo katika maisha yao na hatimae kufa na kukatisha ndoto zao, wako wengine kwakushindwa kuimiri wanajikuta kupata shinikizo la damu, msongo wa mawazo(stress) na wengine kupata mimba na kuiharibu na hata wengine kuitwa mama wakiwa wadogo na wengine hata kuthubutu kutoa kujiua.

Katika dunia kumekuwa na mitindo mingi(style) za namna ya kumtega mtu ili kumpata na hatimae awe mpenzi wako (mwanamke au mwanaume wote wanaweza kufanya) na hivyo watu wamekuwa na bidii katika kujifunza na bidii katika hilo……..ndoma mambo yote yahusiyo mapenzi yanamvuto mkubwa katika jamii yetu iwe muziki au vitabu na hata majarida mambo yote haya yanajaza katika akili ya watu na watu kuyafanya kuwa ni maisha yao.

Mbaya zaidi waliowateule wamechukua nafasi katika kujinza namna ya dunia inavyofanya na hata kuwa waumini wakubwa wa mambo hayo kuliko hata wanagiza kusema na kuona kwamba upepo wa dunia umekuwa na nguvu hata kuliko upepo wa Mungu…………..hapa na zungumzia upepo kama mambo yahusiyo dunia yamekuwa na ushawishi mkubwa kuliko mambo ya nuru.

Ni kisema usiyatazame nitakuwa muhongo lakini kubwa ningependa kujua kwa ufasaha zaidi wa mambo yaliyo bebwa na dunia kuwa hatima yake ni KUKUPOTEZA KATIKA KUHATAMIWA NA MUNGU! Lazima ujue yaliyo ndani ya Mungu hayo mengine utayajua kwakua ndani ya Mungu kuna hazina ya kutosha.

Ukienda kinyume na dunia kunauwezo mkubwa kwenda sawa na Mungu lakini ukienda kinyume na Mungu ni wazi utakuwa kinyume na Mungu ndoma dunia inakumeza kwakua uko nje ya utawala wa Mungu.

Ni vizuri uweke maisha yako SALAMA  kwa Mungu ndio asili ya USALAMA na penda ni kuhakikishie hakuna aliyeyaweka maisha yake katika mikono salama ya Mungu na mwisho akashindwa KUSTAWI,

Imeandaliwa na;


Cothey  Nelson……………………………………………0764 018535

Alhamisi, 14 Mei 2015

JANA INANISUMBUA



JANA INANISUMBUA,


 Ni rahisi kujikinga kwa jambo ambalo alijatokea kuliko jambo ambalo limeshatokea ndomana watu usema KINGA NI BORA KULIKO TIBA, wakati mwingine  mtu anawezafanya jambo ambalo hajui kwa uhakika hasa matokeo ya jambo hilo ndomana mwisho wa jambo unaweza kumkuta mtu anasema laiti NINGELIJUA! Ni singelifanya jambo kama hili hasa kwa jambo baya ambalo linamfanya mtu moyo wake kuwa chini.

Wako walikatika NDOA wanalia na kujuta kuolewa au kuoa na mtu wanaoishi nao wako watu wanaonabora wangekaa kama walivyo tu pasipo kujihusisha na jambo lolote hasa katika swala la mausiano…. mathalani katika NDOA mwenzi moja anapokosa kuwa mwaminifu na kumletea mwenzie magonjwa mfano UKIMWI(ushuhuda wa kweli) mwanamke aliambikizwa na ugonjwa huu na mume wake kutokana na kushindwa kuwa mwaminifu, na mwengine anaolewa na mtu mwenye uwezo mzuri ajui msingi wa fedha zake lakini mwisho wake anakuta mwanaume au mwanamke anakamatwa kwa tuhuma za madawa ya kulevya au jambazi.

Sio hao tu pia wapo wafanyakazi wengi wanajuta kwa kufanya kazi mahali wanapofanya kazi mathalani wasichana wanalazimishwa kufanya mambo ambayo kwa uhalisi wake anajua sio haki mathalani kuwa dhurumu watu kuandika taarifa feki na kusababisha mateso kwa mtu na familia yake na wako watu ambao waliomba kazi wakitegemea au kufikiri kazi hiyo ni halali na kile kinachotambulishwa na hiyo kampuni kumbe sicho anajikuta kujiingiza katika hali ya ubazilifu wa mali ya umma mbali na hayo wako mabinti na vijana wengi wakipoteza ndoa zao kwa sababu ya mabosi zao.

Ni seme wazi katika hili JANA INANISUMBUA ni kweli jana inaweza kukusumbua kunaweza kuwa katika katika UJINGA WA MTU au MSUKUMO USIOKUWA UTAYARI BINAFSI na hatimae kupelekea maisha yake kuwa kama jinsi yalivyo.

Mathalani ajari inamkuta  mtu na kupoteza baadhi ya viungo vyake mathalani macho,miguu na hata mikono na kusababisha yale aliyokuwa anayafanya kushindwa kuyafanya tena kutokana na utofauti aliokuwa nayo hili ni hali isiyohusishwa na utayari wa mtu…..niseme neema ya Mungu izidi kuwa juu yako!

Tundwe mbele na kurudi nyuma tuseme kila jambo ambalo limekufanya uwe hapo ulipo leo lazima na liweke kumbukumbu katika maisha yako inaweza kuwa ni njema ikazidi kukupa matumaini au mbaya ikazidi kukupa huzuni pindi unapoliikumbuka tu………na wakati mwingi katika jambo baya limesababisha msongo wa mawazo (stress), kubwa sana inatubidi tutafute suluhisho ili maisha yaendelee na sio kwendelea tu katika hali njema yenye ubora wake!

MWANGA WA MUNGU!

Ukweli tunamwihitaji Mungu wakati wote ili mradi maisha yanaendelea na hata yasipo ondolewa, unaweza ukajitaidi sana kumudu katika akili zako na hata kutumia taasisi katika kukushauri bado utakuwa na chembechembe katika ufahamu wako,

Na bado katika hali tumeona wako watu wamekuwa wakishindwa kumudu na hasa mambo mengine yanapoongezeka na wengine upelekea katika kujinyonga au kujiua katika namna nyingine yoyote………inasikitisha kwakua wengine walikuwa na potential katika kuisaidia jamii katika kuwatibia hama kuwaongoza katika kuwafanikisha katika hatima zao.

Mwanga ulijaa Mungu ndio suluhisho la kudumu mathalani akili iliyomjaa Mungu mathalani YUSUFU alimuona Mungu katika kila jambo alilokuwa akilipitia haijalishi ilikuwa inapicha hipi katika jamii inayomzunguka yeye alichokiangalia ni namna Mungu anavyhusika katika maisha yake!

Mungu ndiye aliyekuwa na spea zote za mwili wako na ndiye anaweza anaweza kurekebisha kila kitu au spea zilizo athirika na kuzifanya ziwe bora, amua kumfanya MUNGU kuwa na nafasi ya kipekee katika maisha yako kwa kumfuata kwa ukamilifu mbele zake!

Imeandaliwa na;
Cothey  Nelson………………………………………………………0764 018535

Jumanne, 12 Mei 2015

MAUSIANO SALAMA-7



MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA MAUSIANO YA KIMAPENZI;


ASANTE….mpendwa msomaji kwani tangu tulipoanza katika somo hili linahusu MAUSIANO ikumbukwe kuwa sikuandika ujumbe ili kuchochea watu waingie katika mausiano katika hali ya kukulupuka au kuharakisha mausiano…..bali kutokana na mateso na vifo na maisha ya majuto yanayo wa kumba watu walio katika MAUSIANO kwa ujumla wao BABA,MAMA,KIJANA na hata MTOTO…kubwa kuliko yote nikuhusishe WEWE BINAFSI UJIWEKE KWA MUNGU.

Unaweza sema mbona usiano wa watu wa nyuma ni tofauti kabisa na sasa kwani mwanzo mausiano hayakuwa na matatizo kama hivi sasa….. bali ningependa kukutoa katika mawazo hayo kukukwambia matatizo yalikuwepo japo yalikuwa ni tofauti na mateso yalipo sasa hivyo si jambo la tofauti sana kwani kadili nyakati zinavyobadilika ndio mambo mengine yanavyobadilika.
                                                     
                                        V.KIBALI CHA MUNGU
Hili ndio hitimo sahihi kwa mtu ambaye anamwamini Mungu kwa dhati na kuruhusu maisha ya Mungu kuishi ndani yake katika hali ya ujazo wa kimungu uliokamili. Ni seme tu hatua hii sio lelemama kwani namna ya kuenda na jambo ni ngumu sana kwani wakati mwingine inaweza kwenda kinyume kabisa na AKILI yako.

Kwa kifupi haya ni mausiano ambayo uwa kwa asilimia zote 100% yana dumu sana kuliko yote lakini jambo hili si rahisi na kwa kusema hivi haina maana kuwa hamtatofautiana wala kupishana la asha yote yatatokea na hata kuzidi hayo lakini kubwa kuliko yote MIOYONI hawezi kutoana kamwe.

Ni seme hapa ndio ndoa inaanza na inakuwa ya maana sana kwani KIBALI kinaanza kutawala katika kila mnachokifanya kina tawala na neema ya Mungu kwa asilimia zote na machozi yenu yana kuwa machozi ya Mungu mwenyewe na hata furaha yenu inakuwa furaha yake na hapo ndio fursa nzuri ya vipawa na huduma ambazo ameziweka ndani yenu kuanza kufanya kazi katika ufanisi mkubwa.

Wakati mwingi katika kibali cha Mungu kinaweza kisiwe kibali katika macho yako na endapo nguvu ya macho ya nyama yakawa yananguvu kuliko macho ya rohoni ni wazi kupata na kudumu katika kitu sahihi si kitu rahisi.

Mungu uwa anangalia sana wakati wa mwisho kuliko mwanzo kwakua katika mwisho mzuri ndio ujenga ushuhuda ulio bora na wenye maana sana kwa Mungu kwani katika yeye kuna kila kitu ambacho wewe unakihataji.

Ni muhimu kutambua kuwa MUNGU ANAKUPENDA KULIKO VILE UNAVYO ZANI kwakua yeye alikujua na hakika aliyekutunza tangu awali na kamwe hawezi kukuacha uhaibike alipokuumba hakuwa na JAMBO baya nawe kama ukiamua kumfuata na kumsikiliza kamwe hauta weza kushindwa kufika SALAMA!
Yeremia 29:11
Najajua mawazo ninayo wawazia ninyi sio mabaya bali kuwapa tumaini siku zenu za mwisho!!!

Imeandaliwa na;
Cothey  Nelson……………………………………………0764 018535


********************MWISHO**********************

Ijumaa, 8 Mei 2015

MAUSIANO SALAMA-6



MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA MAUSIANO YA KIMAPENZI;



Tukiwa tunaendelea katika uwanja wetu wa MAUSIANO kwakua ndani ya ulimwengu wa sasa kumekuwa na tabaka mbili kati waliobebwa na mausiano ya kimapenzi na wasiobeba na mausiano ya kimapenzi bali wanaojiongoza katika utashi wao, na leo tunaingia katika sehemu ya sita (6) kwa hakika tunaelekea mwishoni wa som letu lakini huu mwisho ndio unaokamilisha mwanzo………….kwakua kila lenye mwanzo lina mwisho na basi pasipo mashaka basi lenye mwisho basi lilikuwa na mwanzo……..barikiwa na karibu tena!

 IV.KIBALI KATIKA MOYO WAKO
Hii ni moja ya sababu ya watu walio wengi katika kuingia na kutoka  katika mausiano ya kimapenzi katika hili utasikia kauli nyingi sana mathalani”SIJISIKII KUWA NAE”, “ YAANI MOYONI MWANGU HAYUPO KABISA”, YAANI PALE…. HAKUNA CHA KUNISHAWISHI HANA PESA WALA MVUTO” na mengine mengi ambayo naamini msomaji unayajua kama ujawai kusema moyoni mwako basi umesikia na hata kuambiwa kama ujasikia kutoka katika mtu mwingine.

Na kubaliana kabisa kuwa mausiano mazuri yanategemea sana kibali toka katika moyo wako, na tunapozungumzia hali ya moyo kuwa na kibali na mtu huyo hapo tunazungumzia hali ya moyo wako kulizika nae, lakini changamoto inakuja pale tu sababu za kuushawishi moyo wako katika kuridhika nae zinamsingi wa kutosha katika kuimiri suluba za ndoa  na kufanya uendelee kumpenda na kumuona bora kuliko ulivyomuona jana………hapa ni swali ambalo moyo wako utaweza kujijibu pindi utakaposema ndio au hapana!

Kwakua tumeona watu wengi sana waliwapa kibali watu katika moyo wake na baadae akashindwa kuimiri shuruba za ndoa na mwisho sijui ilikuaje ghafla tukaona amemtoa mtu katika moyo wake na baada ya kumtoa katika moyo sijui lilibaki wazi au nafasi ilichukuliwa na mtu mwingine!

Ndomana nasema kwamba mtu kupata kibali katika moyo wako ni jambo la muhimu sana lakini inaweza isiwe sababu ya kuchipua uhusiano wa kimapenzi kwakua hiyo pekee haijitoshelezi na ukumbuke wewe unakuwa sio wa kwanza lakini mwisho wake unakua tofauti na vile ulivyotegemea kwa maana unahitaji kuwa na kitu cha kukamilisha ikakuweke katika mazingira salama yaliyo na matumaini katika maisha yako ya sasa na ya baadae.

Ni vizuri kuwa makini sana kwa wakati ulionao sasa kwani hatua ikitokea umeikosea basi kinachofuata ni majuto alama ambayo inaweza kuwa na nguvu ya kukurudisha nyuma kila mara utakapotaka kupiga hatua ya kuleta maendeleo katika maisha yako.

Katika hatua hii kunaweza kukupelekea kuwa tajiri au kuwa masikini uliokithiri na sijui utamlaumu nani? Lakini katika mzuri unaweza kujipongeza katika maamuzi ulio ya chukua lakini unahitaji wewe kuyabeba maisha yako na sio maisha ya kubebe wewe kwakua yenyewe hayajui kule unatakiwa kwenda bali wewe katika hali stahili unajua ulikotoka na unamalengo mema katika kukufikisha hatua moja iliyo na hatima njema katika maisha yako

Imeandaliwa na;
Cothey Nelson………………………………………0764 018535