Ijumaa, 27 Februari 2015

UWEZA ULIONDANI YA MUNGU




UWEZA ULIONDANI YA MUNGU;



Katika ulimwengu tulionao sasa kila kitu kinauwezo binafsi ambao utofautiana  kulingana na utendaji wake na kusudi lake,japo viko vitu ambavyo vinaonekana kuwa vina uwezo mkubwa kuliko vingine kulingana na udhihirisho wake pamoja na muonekano wake.

Uwezo wa mtu au kitu ndicho kinachoamua uishi wapi/vipi au ujasiri wa mtu na uhuru wa mtu kwakua uhuru kwa mwenyenguvu utegemea udhaifu juu ya mwingine.pindi kama wewe sio jasiri basi ujasiri utategemea kwa kitu kingine kitakachokuzunguka ambacho kinakuwa kama kinga katika maisha yako.

Katika dunia ya leo kila mtu utafuta mahali au kitu cha kujistiri au cha kumwifadhi wako wanajifunza kareti katika kujiami,wako wanaotumia pesa na wako wanatumia nguvu za giza katika kujiami na kujiweka katika maisha ambayo wanafikiri kuwa yanaweza kuwaweka huru lakini wewe binafsi unaweza kujiuliza umejiweka katika kinga ipi?

Uhuru ulionao utegemea nguvu uliyonayo pamoja na ufahamu ulionao kwakua hivi ni vitu kwa uhakika vinategemea sana jinsi unavyojitambua na ndivyo utakavyofanya.

Unapozungumzia UWEZA uwa unazungumzia MUNGU mwenyewe maana hakuna badala yake wala mwenye kuingia ulingoni na kupambana nae lakini swali linakuja mbona hata wanaomwamini 

Mungu hawawezi kuutumia huu uweza ukaleta mpenyo katika maisha ya mtu husika badala tumekuwa tukiona watu wengi wasio na Mungu wamekuwa wakifanikisha mambo yao  kuliko wale wanao mwamini Mungu.

Hivyo swali linakuja kwanini watu wanaomwamini Mungu wa kweli hawawezi kudhihirisha kuwa Mungu walionao ni mkuu sana kuliko kiumbe chochote duniani kwani vyote ni kazi ya mikono yake na wala hakuna kilichojifanya chenyewe!

Japo yako mambo mengi ambayo yanaweka kikwazo katika kudhihirisha uwezo wa Mungu;

•Kushindwa kumfanya Mungu kuwa ni wa binafsi!

Lazima umweke Mungu ni zaidi ya kusanyiko au kikundi chochote haijarishi hicho kikundi unakiamini au haukiamini lakini jaribu kukitoa katika ushirika wako na Mungu japo hicho kikundi kinaweza kuwa cha msaada sana kwako lakini kubwa lazima utofautishe kuwa hilo kundi tu lakini maisha yako na Mungu yanategemeana sana.

Hili lolote linalotokea lisiwe shida katika maisha yako kwakua wako watu wanaumizwa na ndugu zao katika kristo yesu, wachungaji hivyo wanahatarisha maisha yao na Mungu na kuwa hatarini pasipo kujua vyote vilifanyika tu ila Mungu ndio kila kitu( mtendaji na mtoshelevu) analo likusudia ndilo linalofanyika haijarishi mawingu au mvua.

Lazima utambua kundi linapochoka na sio Mungu amechoka au linapocheka na Mungu pia naye anacheka hivi ni vitu viwili vilivyotofauti sana.

Tumemfanya Mungu kama tunavyomuona katika macho ya nyama hivyo ikatupelekea kuenenda kwa jinsi ya Mwili……maana hapo ndicho chanzo cha chuki,mateso,wivu na hata kupendelea.

Watu wengi wengi ambao hawajaokoka uwa wanakuwa makini sana kusiliza kile ambacho wataambiwa na utayari utendaji wa kile walichoambiwa pasipo na hata kujijengea mifano mengine ambayo itakuwa ni mzigo katika maisha ya mtu binafsi.

Tumemweka Mungu katika makundi na ushirikiano tukamleta Mungu kuwa ni sawa na furaha ya muda katika kundi au kusanyiko linalomuhusu Mungu hivyo lolote linaloendelea linakuwa linaathiri na ushirika wako na Mungu likiwa zuri basi litajenga na endapo likiwa baya basi litaharibu ushirika wako na ndio chanzo kimoja wapo cha watu kufungua makanisa, kuama makanisa na hata masengenyo,chuki na kisilani uanzia hapo.

Imeandaliwa na;

             Cothey Nelson…………………………………….0764 018535

Jumanne, 24 Februari 2015

UTULIVU MAJI HAINA MAANA MAJI HAYO NI SALAMA



UTULIVU WA MAJI HAINA MAANA MAJI HAYO NI SALAMA;



Maji yaliyo salama ni kivutio kikubwa katika kuyatumia katika shughuli za kawaida na hata kukidhi haja ya mwili yaani kuyanywa, kwani macho yako yatatoa msukumo wa kufaa katika mwili wako na ujumla wa afya yako itakuwa ni njema hivyo yanafanyika kuwa msaada kwa watu wengi wakitumia maji yaliyotulia yanakuwa ni maji bora.

Ni kawaida ya watu kupenda sana mahali penye utulivu ili kumlahisishia hazma yake au lengo lake ambalo analikusudia, ni kweli mahali penye utulivu panavutia wengi sana lakini swali linakuja je!usalama umeambatana mahali hapo maana mahali hapo jambo la msingi ni usalama kuliko hali iliopo au kinachoonekana.

Hii ni moja sababu ya vijana wengi katika harakati zao katika kumpata mwenzi wake,endapo utakapo wauliza  wote watakwambia na mtaka MTU ambaye ni mtulivu, swala linakuja utamjuaje kuwa huyu ni mtulivu?

Na wako watu walisema mahali hapa ni salama sana lakini baada ya muda tu akaona mahali hapa ni pa chungu na ni pabaya sana kuliko jua la mchana jangwani.pamoja na hali hiyo kuwa kukuta watu wengi yale waliyo yaona ni tofauti na uhalisia ulivyo…….kama ni mnyama mkali basi ameendelea kula watu pasipo watu kujielewa au kutambua.

Ni kweli maji yaliyotulia yanakadiliwa kuwa yana wanyama wa majini kama mamba lakini unapoona maji lazima utambue ni aina gani ya maji kwani mamba hapatikani kila matuo ya maji bali upatikana katika maji yasiyo na chumvi, na kila aina ya maji kunaviumbe tofauti wanapatikana hapo mathalani maji ya chumvi utamkuta papa, na kila aina maji maandalizi yako yatategemea aina gani ya mnyama anapatikana hapo na pindi utakaposhindwa kubaini aina kiumbe kinachoishi mahali hapo basi maandalizi yako hayataleta matokeo unayoyategemea.

Ni wazi katika mtego huu anayeweza kupona ni kipofu tu na sio mtu mwingine kwakua katika hali ya utulivu kila mtu upenda kuwepo hapo hata bila ya kujua huo utulivu ni wa kudumu au wa muda mfupi tu kwakua kuna kuwa na ushawishi wa macho na kusikia lakini kwa Yule kipofu kuamua kitu gani kifanyike inahitajika sana hali ya kujiridhisha ya hali ya juu sana na sio kukupuka katika ushawishi usio kuwa na kina katika ya ustawi wa maamuzi yake ulio na mwanga wa uhakika.

Imeandaliwa na;
     
             Cothey Nelson………………………………………..0764018535