Ijumaa, 10 Oktoba 2014

MUUNGANIKO WA AJABU



USTAWI WA MTI UTEGEMEA MIZIZI;



MAFANIKIO YA MKRISTO UTEGEMEA SANA MUUNGANIKO WAKE NA MUNGU

Ukiona kitu kina nguvu au kiko imara basi jua nyuma ya hicho kitu kimeshikwa na chenye nguvu kinachoishikilia. Unapoona jambo la kifahari na la ajabu analolifanya mtu ujue nyuma kunauwezesho wenye nguvu.

Kila mtu anayependa kufanya mambo ambayo watu wanapoona watashangaza na kustajabu na kumpa pongeza na kuonyesha kuwa amefanya jambo la maana sana lakini matarajio yako yanabebwa sana na kile ulichoshikiliwa sana.

Hakuna mtu upenda kuvaa masazo( out of fashion) au kukaa mahali ambapo hapampi heshima au apafurahie bali utegemea kile alicho ungamanishwa nacho kinauwezo wa kumweka hapo au akiwezi, hivyo matarajio ulio nayo yanabebwa sana na uwezo uliokushikilia.

Ukisikia huyu anasoma uingereza, nchi tofauti anapozaliwa (Africa) na huyu anasoma shule iliyo jirani yake lakini yote haya ubebwa na nguvu iliyo nyuma yake yenye uwezo wa kukufikisha hapo ulipo.

Mafanikio ya mkristo utegemea sana na jinsi alivyo imarisha misuli yako katika yeye
 ( nguvu ya muunganiko katika yeye)
Kutoka 19: 5

Kama vile uimara wa mti utegemea sana uwezo wa mizizi ndivyo ustawi utegemea sana jinsi uliimarisha mizizi yako katika yeye.

Lazima ujue kuwa bila ya kusimika mizizi yako katika wewe hauwezi kuwa imara katika yeye na hatimae ukapate mafanikio yake.

Ni vizuri utambue kuwa kunamafanikio na kufanikishwa, hivi ni vitu viwili ambavyo haviwezi kuchangamana hata chembe kwa kila kitu kina kitu kimeshikiliwa kinaweza kuwa na nguvu au hakina nguvu.

Ninapozungumzia mizizi katika Mungu ninazungumzia nguvu ya kumsikia Mungu na kumwelewa na hatimae kuingiza katika utendaji. Kumwelewa kunadhihirika katika utendaji maaana ndio ishara ya kuonyesha kuwa umemwelewa na unamwamini na kumtegemea.

Bila kuishi na Mungu na kumsikia wewe binafsi ni ngumu sana kwa wewe kufanikishwa na Mungu kwani yeye amebeba utoshelevu wako kwa ukamilifu.

Mungu ndio anakupa utajiri na kukustarehesha kwakua vyote viko kwake, usitafute kujistarehesha bali tafute akustareheshe kwakua starehe yake haina majuto wala maswali iko na amani iliyostahiki iliyo jaa utoshelevu wake.

Hauhitaji kutafuta wapi mali zipo bali mtafute mwenye mali ili yeye akufanikishe kwa kuwa vyote ni mali yake na vinatoka kwake.

Ukifanikiwa katika kumsikia yeye kuliko chochote basi unakuwa katika nafasi iliyo sahihi ya kuwa vile anavyotaka.

Usivitegemee vya Mungu kuwa vyako kama wewe ujawa wa Mungu kwanza ndivyo vyake moja kwa moja vinakuwa vyako.


Imeandaliwa na ;
                           Cothey Nelson, 0764018535, cotheyn@yahoo.com


Sina maneno mengi zaidi ya kusema Asante!!!