Ijumaa, 14 Septemba 2018

SWALI LINAKOSA MAANA!




Kama binadamu uliopata neema kuingia katika mifumo mbalimbali ya elimu na kufanya mitihani, utakuwa ulishakutana na maswali katika mitihani yaliyokosewa au yasiyo na majibu!

Wakati mwingine swali lililokosewa uweza kurekebishwa ili liwe na MAANA au kubadilishwa na pengine kutoa alama za bure (free masks) ikiwa hilo swali alikujulikana mapema wakati wa mtihani ila baada ya kusahihishwa mtihani likagundulika.

Karibu!!!

Maswali yamekuwa ni rafiki wa akili na hasa katika kupasha joto ubongo, na upelekea hali nzuri kwa akili kupanuka na kupata uelewa mwingine.

Na wakati mwingine mtu anapokosa jibu hali hiyo uweza kuingia ndani ya moyo na kuleta usumbufu, usumbufu wa mtu kuwa na maswali mengi kwa kile kinacho mkabili pasipo kujua niende kushoto au kulia, hali ya swali kuwa na jibu zaidi ya moja na hatimaye kushindwa kupata jibu linalojitosheleza na hata kujikuta uko njia panda.

Pindi inapotokea mtu anapokuwa na maswali mengi kichwani mwake kwa kiasi kikubwa inategemea hulka ya mtu husika wako watu wanapokuwa katika hali hii upenda kucheza mziki, au kupiga makelele,kuongea sana, kukaa kimya na mwingine upenda kulala hama kulewa na mambo mengine yafananayo na hayo lakini bado unaweza kukosa jibu sahihi au lililojitosheleza katika swali husika.

SWALI LINAKOSA MAANA PALE UNAPOPATA JIBU!

Kama samaki anapo poteza makeke yake au usumbufu wake ni pale utakapo fanikiwa kumtoa nje ya maji na kumweka nchi kavu………………………………………………..!

Ndivyo ilivyo pindi utakapopata majibu katika maswali yanayo kukabili hapo akili uweza kutulia na hali ya ushwari uweza kuingia ndani ya moyo wako.

Ndomana waswahili usema “ atafutae achoki na akichoka amepata” hivyo utashangaa pindi mtu atakapo choka wakati ajapata japo yote yanawezekana kutegemea na hali ya ndani ya mtu husika .

Na wakati mwingine unaweza pata majibu lakini sio utatuzi wa leo wala kesho bali utakuweka katika hali njema ya matarajio ya uhakika wa kweli katika majira yajayo.

Usiruhusu maswali yawe maisha yako maana yatautesa ufahamu wako! Bali tambua kwa kila jambo/swali linalokuja katika maisha yako uwa tatizo linaisha ni mpaka ujue majibu ya maswali hayo yanapatikana wapi? Maana ukikosa kujua sehemu husika hauwezi pata majibu ya uhakika.

“ hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea”

1 Wakorintho 10:13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.

Endapo ikatokea ukakosa majibu ya maswali yako kwa wanadamu ( watu unao waamini) usihofu wewe fungua hazina ya mbingu hiyo uwa haikosi majibu maadam mbingu hipo basi mwenye mbingu yupo na majibu yapo.

Haya ni majibu yanayoleta amani ya kudumu, maana hicho ndicho chanzo sahihi cha majibu ya maswali yako.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………………0764 018535