Jumanne, 26 Januari 2016

UNATAKA KUWA NANI?




UNATAKA KUWA NANI?




Kama kuna swali rahisi kujibiwa na watu wengi pasipo kujali umri, rika na hata jinsia ni pindi utakapotaka kujua MTU anataka KUWA NANI? Ni swali ambalo watu wengi upenda kusikia kutoka kwa mtu japo wakati mwingine mtu anaweza asiwe radhi kuzungumzia ndoto zake au matarajio yake hadharani. Japo WEWE UNATAKA KUWA NANI? Ni swali kwa hakika utapata majibu mengi kwakua kila mtu upenda kuwa mtu fulani katika jamii ya sasa hili,kwa uhalisia,  swali hili alitajibiwa na watu wa aina fulani tu bali itakuwa ni watu wa rika zote si watoto ,vijana wala watu wazima kila mtu anakuwa na shauku ya kuwa mtu fulani katika kipindi fulani kijacho.

Kwa vijana wamekuwa na muamko wa kipekee katika kutaka kuwa sawa na ndoto zao zilivyo na wakati mwingine wamekuwa wakipenda kuwa na wenza ambao utaendana na ndoto zao au unaweza kukuta kijana anataka aolewe au aoe mwanasheria,daktari,muhasibu,engineer,mwalimu na wengine mengi  wako vijana wameenda mbali sana wakitaka aina fulani ya wenza wao atakama anataaluma anayoitaka pia upenda kuona awe na muonekano fulani,rangi fulani ili aweze kuwa na mvuto zaidi katika maisha yake.

Kuna swali ambalo ni rahisi zaidi ya swali la mwanzo lakini ugumu unakuwa katika kusimami katika yale unayo yataka….. swali lenyewe unaweza kuulizwa  JE! UNAYAPENDA MAISHA YAKO? Hili swali ambalo ukimuuliza mtu, kwa haraka haraka anaweza kuona kama unamdharau au unamkejeli ikiwa rafiki yako utafanya awe na swali lingine pindi utakapoamua kumuuliza swali hilo kwanini kaamua kuniuliza swali hili je! Kunautofauti gani kati ya mwanzo na sasa. Lakini wako wengine watapuuzia tu na kusema naona kuwa hauna swali la maana.

Ni ukweli usiopingika kuwa unataka kuwa nani na namna unavyoishi vinaenda sambamba japo najua kunauwezekano(exception) utendaji unaweza kuendelea ambao utakuwa nje ya akili za kawaida yaani pasipo mipango yako, viko vitu vitatokea na kujikuta unafanya jambo na linatokea sawa na vile linapaswa kutokea mathalani daudi Mungu alipomuandaa kuwa mkombozi wa Israel alijikuta anapambana na dubu , mwanasimba na wanyama wengine na anajikuta anawashinda na hatimae mwisho anakuja kupambambana na Goliathi na hatimae kuwa mkombozi wa Israel.

1 Samweli 17:37 Daudi akasema, Bwana aliyeniokoa na makucha ya simba, na makucha ya dubu, ataniokoa na mkono wa Mfilisti huyu. Sauli akamwambia Daudi, Enenda, na Bwana atakuwa pamoja nawe.

Kuyapenda maisha yako hilo ni jambo la kawaida sana lakini kubwa sana ni kweli unayaweka mwingiliano na vile wewe unataka kuwa au kunamuachano wa vitu viwili vilivo na mwelekeo tofauti lakini vina shabaha moja,ni seme wazi kuna kuyapenda maisha na kuyathamini maisha japo kwa uhakika unapozungumzia kukipenda kitu hakuna utofauti na kukithamini hicho kitu lakini katika uhalisia wake wake utofauti upo mtu anaweza kuyapenda maisha yake lakini asiyathamini mathalani mtu anaweza kupenda maisha yake lakini ukakuta bado anavuta sigara,bangi na madawa ya kulevya na mengine mengi lakini katika moyo wake anasema anayapenda maisha yake.

Wapo wengine watasema mimi maisha yangu nayapenda lakini sinauwezo wa kuyahudumia ipasavyo kwani baadhi ya vitu sina uwezo wa kuvipata hivyo yanipasa ni ishi kwa shida hivyohivyo mathalani mtu anakula mlo moja kwa siku tu na tena chakula kilekile na sio kwamba anapenda bali ni hali halisi anayoiona katika macho yake kuwa hivi ndivyo ninavyopaswa kuishi.

Na ni ukweli watu wengi wamekuwa wakiishi tofauti na ndoto zao japo mtu huyo anapenda kutimiza ndoto zake mathalani unaweza kukuta mtu mwimbaji anataka kuwa mwimbaji katika hatua kubwa hata ya kimataifa lakini utakuta afuati utaratibu wa kufika hapo kama vile uvutaji wa sigara, unywaji wa pombe, matumizi makubwa ya vitu vya mafuta, kutopata muda mzuri wakumzika ,kutofanya mazoezi katika kupata pumzi ya kutosha ,kutojua namna sahihi ya kutumia sauti yake katika kuifanya izidi kuwa bora siku hadi siku. Na wakati mwingi mtu kwakutokizingatia katika hatua za kukufanya kuwa hatua bora uweza sasa kuwa laumu watu na kusema awapendi maendeleo yake.

Baadhi ya matarajio ya watu wengi ni kuwa na familia bora na kuheshimiana, na mtu uweza kuamasika zaidi pindi anapoona watu wengine wakiwa katika furaha katika ndoa zao pamoja na hayo mtu anashindwa kujua hivi vitu vina maandalizi yake toka matumizi ya ujana wao,  katika starehe zako uweza kusababisha maisha yako ya ndoa kuwa na raha au kuwa na shida, wako watu wameharibu maisha yao ya ujana kwa kiasi kwamba uwezi kushika mimba tena au mwingine kupata magonjwa yakawa ndio maisha yake.

Niseme tu uwezi kuwa unatakata kuwa mcheza mpira maalufu katika dunia ya sasa na huku ukijibidisha zaidi sana katika kujifunza staili za kucheza muzuki………. unaweza kuishi maisha ya katikati usijione kama unaenda mbele au unarudi nyuma hama uko hapohapo.

Unataka kuwa nani sio swala la kusema tu ni swala lakuruhusu na kuamua kuwa humo siku zote katika ufanisi na ubora unaotakiwa sio kujaribu tu na baadae ukaacha.

Swali ambalo na kuacha nalo ni hili tu unataka kuwa nani na unaishi maisha gani?

Imeandaliwa na;

Cothey Nelson………………………………………0764 018535