Jumanne, 7 Novemba 2017

URAFIKI NA NENO





Urafiki ni jambo linalopendeza sana katika maisha ya wengi, kwani hutashangaa kusikia mtu akijivunia sana mwenzake! Ukimuuliza vizuri kwanini unampamba sana na kujivunia sana mtu huyu bila shaka ataongea kwa bashasha uku akijiamini na kwa furaha akisema “ huyu ni rafiki yangu sana, yaani ninapo muona huyu atakama naumwa nitapona ghafla” naam hakuna kitu kizuri kama kuwa na mtu ukatambua yeye ana upendo wa dhati na wewe, unajisikia uko salama zaidi ya pepo.

Kwakua unatambua ndani ya urafiki wa kweli kuna kusikilizwa, kusaidiana, kurekebishana, kutunziana siri, kuchukuliana na zaidi kunakuwa na kifo cha ubinafsi (umimi) ambao watu wengi upenda sana kwakuwa kila mtu ujiona si bora kuliko mwenzake.

Karibu!!!
Ni rahisi kuwa rafiki wa watu waliookoka kanisani (ukitaka) kuliko kuwa na urafiki na mwenye kanisa ( Mungu) kwa kuwa kila urafiki una utaratibu wake.

Na ni rahisi/inawezekana kufahamiana na watu wengi mahali ulipo ( kanisani, kazini (ofisini) na hata mtaani kwako ) kuliko kuwafanya watu hao kuwa marafiki.

Na ishara kubwa ya urafiki wako na mtu ni namna anavyo husika na wewe kuhakikisha unakuwa katika hali nzuri unayotakiwa kuwa nayo wakati wote maana furaha yake inakamilika anapoiona furaha yako.

Na unapojua una urafiki na mtu ujipangi sana katika kumwambia kitu kilicho ujaza moyo wako na hata rafiki yako atakapo kusiliza hatakuwa makini na kile utakacho mwambia tu bali ataweka mkazo zaidi katika urafiki wenu maana huo ndio utakuwa msukumo wake katika kukutendea.

Urafiki na neon karibu sana!
Inawezekana ukapata neema kulifahamu neno la Mungu ( kuwa kimeandikwa nini? Na kwanini) na hapo ukajua kuwa Mungu anaweza mambo mengi ( kuinua, kuponya, kufariji na mengine mengi) mathalani ukasoma sehemu ambayo bahari ya shamu iligawanyika kwa uweza wa Mungu kupitia fimbo ya musa  lakini hilo neno likikosa shirika nawe (lisibadilishe akili yako na kugeuza mfumo wa maisha yako) unaweza usijue maana yaw ewe kuelewa.

Na watu wengi walioishia katika hatua hii utoshangaa kuona ameacha wokovu au analegalega katika wokovu ( wokovu usio na matunda).

Unapoamua kuwa na urafiki na neno hii ni kitu kingine ni zaidi ya wengi wanavyozungumza au kuamini bali ni namna ya kiungu inayo jidhihirisha kwako.

Kama ilivyo katika urafiki mwingine unavyokuwa huru kumwambia chochote au kumwachia kuyafanya yale ambayo wewe ungeyafanya….. hivyo unapokuwa na urafiki na neno ni muhimu pawe na uwezekano wa wewe kuyafanya yale ambayo neno la Mungu lingeyafanya hapa duniani.

Utofauti wa utendaji utapelekea kushindwa kuimarisha urafiki wenu, na mfanano wenu katika utendaji utafanya urafiki wenu kuimarika na kuaminika zaidi.

hauhitaji kujitangaza hama kujisifia kama wewe una urafiki na neno kwakuwa neno lenyewe litakutambulisha na kujivunia wewe hatimaye kupata heshima mathalani mtu anaposhika mimba hauhitaji kutangaza mtaa mzima yenyewe itajionyesha na watajua tu kuwa huu sio ugali.

Ukweli wokovu bila urafiki na neno (mwingiliano usioelezeka) ni ngumu kuona mkono wa Mungu kwa ukamilifu.

Yohana 15:7  Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.

Moja ya mwingiliano usioweza kukatika ni huu, na kwa maelezo mafupi huu muunganiko ndio asili yetu kwahiyo kinachofanyika ni sisi tunarejea katika muunganiko na sio tunaanza muunganiko.

Kadili mwingiliano unavyokuwa au urafiki utakapozidi kuongezeka ndipo hapo utaomba naye atasikia na atajua hitaji lako au ombi lako hata kabla kinywa chako akija tamka na sio kupiga makelele hama maombi ya kubahatisha.

Faida kubwa ya mwingiliano huu (urafiki na neno) akili zako hazita tumika sana bali maongozi ya Roho mtakatifu yatakuwa dira yako.

Ni maisha yenye raha na furaha ya kweli maana ndio maisha tuliyo kusudiwa na Mungu.

Nzuri kuliko yote, huu muunganiko au mwingiliano hauna mwisho ( expire date) ni wa milele.

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………….0764 018535

Jumanne, 31 Oktoba 2017

MAJI YANAKUWA NA MAANA PALE UNAPOKUWA NA KIU







Moja ya bidhaa inayopendwa na watu wote haijalishi ni tajiri au maskini ni MAJI kwani kiu hainaga mbadala kwakuwa hauwezi kula chispi badala ya maji wakati unakiu ya maji na pengine ukiulizwa kwanini unafanya hivyo useme ” mimi ni tajiri” unaweza fanya magazeti wapate habari ya kuandika.

Na unaweza kugundua kumbe sote maji ni muhimu kwetu pale maji yanapo kosekana kwa muda utakuta jamii yote wimbo ni moja “ natafuta maji”………. Unaweza kushangaa tajiri akimsalimia maskini kwa heshima zote “ ndugu habari yako” pindi anapo hisi kupitia huyu hitaji lake la maji litapatiwa ufumbuzi, na unaweza usishangie jamii yote ikakusanyika sehemu moja bila kujali hadhi zao na wote wakihitaji maji.

Na amini siku zote uhitaji ndio uzalisha kiu ya kutafuta, kwa maana nyepesi kama hakuna uhitaji basi hakuna maana ya kutafuta ( maana uwezi kutafuta kitu ambacho hauna uhitaji nacho).

Bidii au kujigharimu sana katika kutafuta kitu udhihirisha thamani ya hicho kitu / umuhimu wake, mathalani uwezi kumkuta mtu mzima anakesha usiku kucha na ukimwangalia unamuona hana raha kabisa na ukimuuliza kwanini uko hivyo akakujibu “ sh. 10 yangu nimeipoteza toka jana naitafuta bado sijaipata” unaweza kushikwa na bumbuwazi na kuzidi/ kuzalisha maswali kichwani mwako kuliko majibu! Lakini ikatokea akasema ” nimekesha usiku kucha kumtafuta mwanangu sijampata mpaka sasa” unaweza kujua kuwa hiyo ni kawaida ya wanadamu na hasa mzazi/mlezi mwenye mapenzi ya dhati kwa mwanae.

Japo maji ni muhimu sana katika maisha ya mwanadamu, yakiwepo unaweza usione huo umuhimu wake lakini yatakapoanza kukosekana hapo ndipo utaanza kuona watu wakianza kuumiza kichwa jinsi gani wanaweza kupata maji ya kutosha ili kukidhi mahitaji yao.

Mng’ao wa kitu utegemea sana uhitaji wake! Kitu hata kikiwa na mng’ao gani kama akita tafutwa /hitajika basi jua huo mng’ao utafifia tu.

Pia inawezeka kuna kitu mwanzoni ukikipa thamani kwasababu yakutojua matumizi yake ukakipotezea, lakini pindi utakapojua jinsi kinavyoweza kukidhi uhitaji ulionao taratibu utaanza kukipa thamani ndani ya moyo wako.

Popote ulipo uhitaji wako utakapoanza kuongezeka utaanza kukumbatiwa na ikatokea uhitaji wako kuanza kupungua basi hapo utaanza kuona uhuru wako unaanza kuongezeka basi ni muhimu ujue hiyo ni ishara mbaya mathalani umechelewa kazini bosi akuulizi, umefanya kazi vibaya haulizwi wala hausemwi, uko nyumbani umezidisha chumvi kwenye mboga wanakuangalia, umeunguza chakula kila mtu ajali ni muhimu utafakari kwanini hivi?

Pindi utakapoamua kuwa hitaji la wengi ndipo hapo neema ya Mungu itazidi kukutawala na ongezeko lake ndani yako litakuwa kubwa na kukupa wepesi katika utendaji wako.

Kuwa sehemu yenye staha na viwango vya ajabu kama ukatambua ahutajiki mahali hapo inakuwa na sawa na nzi kuwa katika jagi la maziwa, na uzuri watu wanao uona wewe unaona giza tu, na pengine unaweza kujuta kwanini uko hapo? Ni bora usingeli kuwepo.

Uhitaji mzuri ni pale utakapo jitambua mwenyewe kuwa mimi ndio hitaji la mahali hapa na kuanza kuwajibika kuliko watu kutambua uhitaji wako alafu wewe usijitambue unaweza kuzaa maumivu kwa watu.

Mwendelezo wa uhitaji wako haupimwi na mtu yeyote bali unapimwa na yule aliyekufanya kuwa hitaji sehemu husika, maana pana uwezekano wa kujisikia upo chini pindi watu wakapoanza kupima uwajibikaji wako.

Unapotambua kuwa wewe ni hitaji la watu hawa hama mahali hapa basi ujue Mungu amekuheshimu na kukupa neema yake huna haja ya majivuno bali ni muhimu kuzingatia kuwa hao watu ni hitaji kwako pia ( mnahitajiana).

Ni jukumu lako kuhakikisha kuwa uhitaji wako unazidi na sio kupungua!

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na;

Cothey  Nelson…………………………………………….0764 018535

Jumanne, 24 Oktoba 2017

TESO LA MUUNGANIKO.





Unaweza kukuta mtu ameinamisha kichwa chini na machozi yakimtoka hama kumlengalenga nawe ulipo muona ukaingiwa na huruma na maneno kuanza kutoka kinywani mwako uku ukitafuta namna gani ya kumrudishia raha/furaha yake……… unaweza jikuta unaongea mpaka mate yanaanza kukauka lakini ya mtu haibadiliki na hali aliyonayo lakini ghafla  likatoka neno kinywani mwako lililo unganika na jambo lililopelekea kukatika kwa maji machoni (machozi) hapo ndipo unaweza kukuta anaanza kuinua kichwa chake kukutazama kwa macho yake yaliyojaa maji ya mwili.

Na ni kawaida pindi unapotaka kuuangusha mti katika ukubwa wowote ni lazima uende kwenye kiunganishi kilichopo kati ya mti na ardhi kwa lugha rahisi ni mzizi, kinacho safirisha maji kutoka kwenye ardhi na kuelekea kwenye shina hatimaye kusambaza katika mti mzima na pindi unapofanikiwa kukata muunganiko huo huna haja tena ya kuwa na wasiwasi ujue tu mti utadondoka.

Huna haja kukesha usiku kucha kutafuta m baya wako ni nani? Ni muhimu kutambua kile ulichounganishwa ndicho kinachokutengeneza, hivyo huna haja ya kusumbuka na muonekano wan je bali angalia kilicho ung anika nawe na kukutengeneza vile ulivyo.

Wakati mwingine unaweza kushangaa kwanini huyu anafanya vizuri na huyu afanyi vizuri, unapoamua kutafuta sababu ipi ikapelekea utofauti wao ni muhimu uangalie muunganiko wa kila mtu hii inaweza kuwa ni hatua bora sana katika kupata jibu lililo sahihi kuliko kukaa na kuponda hama kukosoa tu.

Wazazi wengi wanapata tabu sana juu ya watoto wao na kuishia kutoa maneno makali pamoja na kuwapiga sana pasipo kutafuta nini watoto hawa wameungamanishwa nacho kinacho wafanya wawe hivyo, maana ni wazi usipojua nini kimeungamanisha mpaka kinapelekea mtu huyu kuwa hivi, unaweza ukashinda usiku mzima na hata miaka bila kupata suluhisho lolote ingawa unaweza kujipa matumaini kuwa labda kesho mambo yatakuwa sawa.

Kwa mtu aliyejiungamanisha na kitu sahihi ni ngumu kumuondoa hapo hata ufanyeje/ iweje atabaki kuwa salama tu maana ule muungamaniko utamnawilisha na kupingana nae ni sawa na kukata matawi katika mti ukitegemea huo ndio mwisho wa mti pasipo kujua shina na mizizi ikiwa salama basi ujue mti uko salama kwa wakati wake utachipuka tu.

Huna haja ya kulaumu/ kujilaumu maisha yako bali angalia sana ni nini ulichoungamanika nacho je! Kinaleta uzima au mauti katika maisha yako.

Unapokuwa makini na kile ulichoungamanika nacho basi hiyo ni ishara nzuri ya kujali ustawi wako kwa kuwa hauwezi kustawi inje ya kile ya kile ulichoungamanishwa nacho.

Swala sio kuungamanishwa tu bali unaungamanishwa na nini? Na hicho kitu kinaleta matokeo gani? Na je! Hayo matokeo yatadumu kwa muda gani? Na mwisho wa siku yatakuweka katika hali gani?

INAITWA SIKU! BARIKIWA

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson……………………………………………………… 0764 018535

Jumanne, 10 Oktoba 2017

SAUTI YAKE NDIO NGUVU YANGU.






Tafsiri fupi ya neno nguvu ni uwezo wa kufanya jambo, na mafanikio ya jambo udhihirisha nguvu ulizo nazo…………………………………………………………………!

Sauti, kuna aina ya sauti zilizo ambatana na maneno fulani na pindi unapo yasikia uweza kubadili hali yako nzima ya mwili, unaweza kuta mtu anaacha kula, kuaghirisha safari zake, kuvunjika kwa baadhi ya ratiba zao na wengine uweza kuzalisha furaha hama maumivu kutokana na sauti iliyoambatana na maneno yaliyotoka katika kinywa cha mtu.

Naam kwa asilimia kubwa watu hisia zao (furaha/huzuni) utegemea maneno ya mtu mwingine. 

Unaweza kukuta mtu anasema siku yangu leo ilikua nzuri sana maana nimeyasikia maneno niliyokuwa na yatamani/ nayasubiri kwa muda mrefu nayo yamegusa hisia zangu na kuchangamsha moyo wangu na inaweza kuwa kinyume chake kwa mtu aliyesikia maneno magumu/ asiyo yapenda hama kuyatarajia.

Japo kuwa nguvu ya maneno unayoyasikia kwa kiasi kikubwa utegemea ufahamu wa wako, maneno ni yaleyale yanaweza kusemwa kwenye kundi lakini matokeo yake yakawa tofauti kwa kila mmoja kulingana na hali aliyonayo (hisia); inawezekana huyu akachukizwa sana na mwingine akajifunza kitu.

Na ikumbukwe kuwa unapokuwa binadamu hali ya kutawaliwa na hisia ni jambo la kawaida.

Karibu!

Sauti yake ndiyo nguvu yangu!!!

Unapokuwa duniani kusikia sauti nyingi ni swala lisiloweza kukwepeka lakini nguvu ya sauti utegemea ruhusa ya ufahamu wako/ udhaifu wa akili yako.

Ni muhimu uone/ utamani kuwa nguvu yako ya utendaji ibebwe katika kusikia sauti ya Mungu, kwani;

i.                    Ni sauti pekee yenye kumaanisha kile kinachosemwa

ii.                  Ni sauti iliyobeba dhamira njema na ya dhati

iii.                Ni sauti pekee isiyo na pande mbili (kigeugeu)

iv.                 Ni sauti pekee iliyo kukusudia kukufanya kuwa bora/ wa maana

v.                   Ni sauti yenye kukufikisha kwenye hatma yako iliyo njema.

vi.                 Ni sauti pekee ambayo ukiifuata hauta kaa ujute.

-          Maana unahitaji kufuata njia unayoelekezwa na sio unayoifahamu

Kama una nia ya dhati ya kupata usalama katika maisha yako basi ni muhimu ujenge urafiki na sauti hii, na unaielewa sauti hii kupitia neno la Mungu pekee hivyo ni lazima ulipende na kulipa nafasi katika maisha yako.

Matukio na simulizi za watu zenye kutia moyo na kuamasisha uwa sio msingi mzuri katika utendaji wako katika ufalme wa Mungu. Bali jenga sana ushirika mzuri na sauti hii maana wote walioifuata walijivunia maisha yao.

Japo wakati mwingi kuifuata sauti hii ni kwenda kinyume na mazingira yanayoonekana katika ulimwengu dhahiri, lakini hauna budi kuifuata maana ubora na ushindi uzaliwa hapo.

Unahitaji uwe halisi kwa Mungu na sio kutaka sifa kwa watu ambao wanakuwa na wewe kwa muda mchache na mwingi unakuwa peke yako.

Moja ya sauti ambayo haupaswi kuipotezea ni hii maana ukiipotezea itakugharimu.

INAITWA SIKU! BARIKIWA.

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………………0764 018535