Jumanne, 28 Julai 2015

JICHO LANGU NDIO MAAMUZI YANGU



JICHO LANGU NDIO MAAMUZI YANGU



 Kile ninachokiona ndicho nitakachoamua sio kile ninakachokisikia!

Hakuna kitu kigumu kama maamuzi na hakuna kitu chepesi kama maamuzi ila inategemea maamuzi haya yamebebwa na nini na yanahusu nini?

Katika uwanda wa mwanadamu kuamua jambo ni dhana pana kuna maamuzi yanatokana na kushawishiwa na maamuzi yanayotokana na busara za mtu husika………..mwisho wa siku yote yanajulikana ni maamuzi yaliyo amliwa na mtu kwa utashi wa mtu husika.

Wako watu wameacha kazi,rafiki,jamaa na hata kugombana na wazazi kwasababu ya kuambiwa maneno na kuyaamini na hatimae kuchukua maamuzi ya kuacha hama kuendelea, maamuzi yanayotokana na kuambiwa yamekuwa na nguvu sana kwakua tunaishi katika dunia ambayo hatujui yote hivyo tunahitaji kusikiliza wengine katika kuchukua maamuzi na tunahitaji kuishi kwa amani na ndugu wanaotuzunguka,

Niseme hata kama wewe mwenyewe  uliwai kuamua maamuzi pasipo kushuhudia mwenyewe ila katika ushawishi wa maneno nikutoe hofu wewe si wa kwanza……hata adam alipoulizwa na Mungu kwanini umekula tunda alisema ni huyu mwanamke uliyenipa…..!!!

Japo matokeo yake yamekuwa ni athari si kwao hata katika ulimwengu sasa na mengi yanatupata kutokana na maamuzi ya hawa watu wawili.

Hakuna kitu kizuri kama kuamua maamuzi yaliyobebwa na ushuhuda wa macho yako na sio ushawishi wa upande wanje! Kwakua maamuzi yanakupa nguvu na kukupa ujasiri katika mwenendo wako, ukweli maamuzi mengi tunayo yafanya kiukweli sio katika maamuzi yaliyobebwa na ushuhuda wa macho yetu. Usipende kuwa na maamuzi yakushinikizwa usio na muono wako binafsi kwamba hivi nasikia au kuambiwa mambo ambayo ya na ushuhuda wenye nguvu katika macho au wakimazingira! Pasipo uhakika wako mwenyewe.

Wako watu waliopoteza Baraka zao na ushindi wao kwa kuambiwa na kushawishika na watu wengine pindi mtu husika anapoamua kumshilikisha mtu jambo lake………….mathalani biashara imeenda vibaya wanaokuzunguka au uliomshirikisha anaweza kusema kuwa uliyenaye sio mwaminifu hivyo vunja nae huo mpango kwani hata kuzidi kukurudisha nyuma maendeleo yako na wewe kutokana na usadifu wa mazingira na nguvu ya ushawishi kwa mtu ukaweza kuamua sasa mimi basi acha niangalia upande mwingine!

Maamuzi yaliyobebwa na macho yako…. kiukweli yanakuwa hayana unafiki wala ushawishi wa mtu au chochote kwakua unakuwa na ushahidi wa kutosha sana ambao moyo wako unakushuhudia kuwa uko salama na sifa kubwa katika maaamuzi haya uwa haya ambatani kabisa na uzushi kwakua kile unachokifanya unakiamini.

Haya ni maamuzi yanakufanya kuwa mkweli na kuwa halisi sana katika kile unachoamua na bila shaka dhamira yako inakuwa haina hatia kwakua kile unachokiamua ni kwa ajili ya kujenga wakati wako katika uzuri.

Nipende kusema kuwa hakuna maendeleo ya kweli kama ukiwa unaamuliwa mambo yako nawe kisha unafuata na kamwe hawezi kwenda mbele japo utaongeza miaka!

Maamuzi ya kuaamliwa yanakuweka katika maisha ya utumwa ambao hutaweza kutoka katika utumwa huo kama utachukua maamuzi bila ya kuheshimu maamuzi yako binafsi kwakua wewe ndio unatakiwa kuonyesha unaijali na kuithamini kesho yako.

Bila shaka ukiwa unaendelea na utumwa wa maamuzi sio rahisi kuungamanishwa na Mungu hata kama ahusiki mkumbuke adamu hata alivyojitahidi kujitetea lakini hakusikizwa tena kwakua Alisha kula tunda ambalo Mungu aliigiza lisiliwe lakini yeye katika ushawishi wa mwanamke ambaye Mungu mwenyewe aliluhusu awe nae.

Mungu amekupa akili akaweka wazo na akakupa kuamua hivyo mtendee haki Mungu kwakuendeleza kile alichokianzisha ndani yako!!!

Imeandaliwa na;

Cothey Nelson………………………………………..0764 018535

Jumatano, 15 Julai 2015

CHAKULA CHAKE NI MAUMIVU YA.......................



CHAKULA CHAKE NI MAUMIVU YA MUNGU


 Sote tunajua kuwa chakula ni kitu muhimu sana kwani pasipo chakula uhai uweza kutoka hivyo tunavyokula chakula inasaidia kuustili uhai ambao Mungu ameweka ndani yetu uzidi kuwepo  chakula ni kitu kizuri na muhimu sana  kwani katika hiki tunapata uwezesho wa kuishi na kuona fahari ya maisha yetu katika kukizi mahitaji ya mwili (katika hili mwili unakuwa na nguvu) na kujisikia kuwa ni mtu kama watu wengine!!

Nazungumzia chakula kama kitu cha msingi katika maisha ya mwanadamu kwani mtu anaweza kukosa mavazi, malazi akaishi lakini kamwe sio chakula kinachoweza kusababisha viungo vya mwili kufanya kazi na hata kufanya utendaji wa mwili kuwa mzuri!

Kwa utafiti wangu mdogo binadamu anaweza kukaa siku nyingi bila nguo akawa salama na kuendelea kuishi lakini sio kushindwa kula katika siku hizo na kuweza kuendelea kuishi ila yesu pekee ndiye aliyeweza kukaa siku arobaini bila kula!

Ni kubali wazi kuwa binadamu hatupo kwa ajili ya chakula ila chakula kipo kwa ajili yetu….hivyo hatuna budi kukitumia kwa ajili ya kujenga afya njema ya miili yetu.

Kisayansi wanasema muonekano wa mtu uonyesha au udhihirisha kiwango au ubora wa chakula anachokula.

Ukweli kwamba mambo mengi ambayo yanafanyika katika dunia, yawe mambo mema na hata yasiyo mema mwisho wa yote yanakamilishwa na jambo au kitu kinaitwa chakula kwa ajili ya kuridhisha mwili katika kuupa matumaini ya kuendelea kuishi!!

Wako watu wanashughulika katika maisha yao ya kila siku kwa ajili yao na wengine kwa ajili ya familia zao, na hata kwa ajili ya ndugu na jamaa wanao wangalia…..ukweli ni seme kuwa katika mambo yanayoweza kuumiza kichwa sana kwa mtu mwenye majukumu ya kuwa hudumia jamii inayo mzunguka na hasa familia inayo mtegemea ni pale anapokosa uwezo wa kuwapa chakula!
Mambo mengine yanaweza yaka simamishwa kwa mtu baada kugundua kwamba uhakika wa chakula haupo au ni mdogo…..hata mzazi anapotaka kumpeleka mwanae shule jambo ambalo linampa furaha sana ni kuona kwamba mtoto wake ana uhakika wa kula vizuri tena katika hadhi anayopaswa!

►Ni seme hili ni jambo muhimu sana lakini katika jamii yetu imekuwa ni tatizo hasa pindi uwezekano wa chakula hicho kutopatikana na ijulikane wazi ninapozungumzia chakula rafiki yake mkubwa ni fedha.

Katika kukidhi mahitaji yake binafsi au familia yake mtu anapokosa kuona uwezekano wa kupata fedha kwa njia iliyo sahihi na kukidhi mahitaji ya familia yake lolote linaweza fanyika!

Wamekuwa watu wakiuana kwa ajili ya kupata fedha na kukidhi mahitaji ya familia zao hasa  wenye uwezo huo lakini kwa wengine wamekuwa wakijiingiza katika shughuli zingine kwa ajili ya kupata fedha katika kukizi mahitaji yake na familia yake kubwa ni chakula moja wapo ya shughuli hizo ni ujangili, ujambazi, utapeli na hata ukahaba!

Wengi wanaofanya shughuli hizi sio kama wanapenda bali yote ni katika mbio katika kufanikisha mahitaji katika familia yake na yeye muhusika.

Watu wamekuwa wakiuuza miili yao ili wapate fedha kujikimu katika maisha yao watu hawa wanafanyakazi kama wanapenda lakini ukweli ni mateso katika maisha yake!

Japo wako wengine wanafanya shughuli hii pasipo kuwa na uhitaji huu hasa hawa si wazungumzii kwakua hawa wanahitaji kitu kingine ili kiwasaidie lakini katika wale ambalo hawanauchaguzi hayo yamekuwa maisha yao na zaidi sana yamekuwa ni maumivu ya Mungu!

Katika makusudi ya Mungu katika kumuumba mwanadamu hajawai kufikiria kusudi la mtu kuuza mwili wake ili kujikim mahitaji yake na familia yake….bali yote haya kwasababu mwanadamu ana utashi wa kufanya chochote ila matokeo yake kamwe huwezi kuyabadili yanakuja sawa na ulivyofanya.

Ni pende kusema kuwa bado unanafasi ya kufanya vizuri na kuwa bora kwa Mungu kwa mtu ambaye anaye husika maisha yake katika kuuza mwili wake bado unaweza kuwa bora na kuwa wa maana hata kuliko unavyofikiri.

Chukua nafasi hii kwa wewe unayesoma kuwa mwema kwa watu wa jinsi hii kufanya kuwa duniani ni mahali salama ambapo yeye anahitajika sana na sio kumuonyesha UPENDO tu! Bali aweze kuona YESU kuwa ndiye mtoshelevu wake na sio kitu kingine!

Mungu hajawai choka, hata choka na kamwe hawezi kuchoka kwa mtu anayempenda bila shaka ni wewe!

Imeandaliwa na;
Cothey Nelson…………………………………..0764 018535

Baraka za Mungu zipo kwa ajili yako!!