Jumanne, 26 Julai 2016

ANAITWA MUNGU!



ANAITWA MUNGU!


Unaweza kumwita mwenye nguvu, wa huruma, wa upendo, wa amani, mponyaji, mfariji hizo zote ni sifa zake lakini kamwe haitabadilisha kuwa yeye KUITWA MUNGU! Karibu sana,

Uhitaji kuchoka sana katika maisha utakapoenda katika njia ambayo Mungu amekuagiza kuenenda wewe tambua kuwa yeye anaitwa MUNGU hakuna jambo au hali yoyote ambayo itaweza kuzuia KISHINDO chake kwakua badala yake hakuna na nafasi yake inabaki kuwa yake.

Uwa yeye hazuiliwi ila anaweza zuia! Achoki ila anaweza kukuchosha! Asahau ila anaweza kukusahaulisha! Achelewi ila anaweza kukuchelewesha! Apatoi ila anaweza kukuchelewesha ANAITWA MUNGU!

Haitaji umsaidie ili ufike mapema yeye mwenyewe anajua namna ya kukufikisha! Ahuhitaji kujipenyeza ili uonekane, ila yeye atajidhihirisha nawe utaonekana tu! Tembea katika hatua zake tu utafika tu maana hakuna aliyetembea katika hatua zake akaishia njiani/akashindwa kufika.

Hana uhitaji ndani yake ila mimi na wewe tunaweza kuwa na uhitaji lakini anajua namna ya kukutosheleza pasipo kukwama kwakua unajua njia ya yeye kukupa uhitaji wako…mathalani yesu alipo gundua ana deni ndipo akaamuru mwanafunzi wake kwenda kuvua samaki kisha achukue samaki na kumtoa fedha alafu akalipe madeni wanayodaiwa.

Nipende kusema hali ya wewe kuwa na uhitaji hilo ni jambo la kawaida kwakua katika biblia watu walikuwa nauhitaji mwingi mathalani sara(uhitaji wa mtoto), batromayo( uhitaji wa kuona kwani alikuwa kipofu), mwanamke mjane wa serepta(uhitaji wa chakula) hivyo sio ajabu ya wewe kuwa na uhitaji wowote kwani unachohitaji hapo ni namna  Mungu afanyike njia ya wewe katika kukutoa hapo.

Nipende kusema mahali ambapo akili yako itakosa mwelekeo kwakua umeshatumia njia nyingi lakini bila mafanikio, huna haja ya kutafuta mbaya wako mtazame petro alipo jaribu kuvua samaki usiku kucha bila mafanikio alibaki palepale mpaka yesu alipokuja pale na kutamka NENO hivyo uhitaji kutembea tembea huku ukiangalia labda huyu atanihurumia lakini tambua kwa kila uhitaji una njia zake za kupata au kukizi uhitaji kwa maana rahisi hakuna mtihani ukakosa majibu, japo wakati mwingine unaweza usipate majibu lakini mtunzi wa mtihani anayo majibu.

Muono wa watu kuona  kuwa umeshindwa sio kweli kuwa umeshindwa, kwani kushindwa kwa mwili sio kushindwa kwa roho na nguvu ya mkristo iko ndani ambayo ndio inazalisha kunawiri katika muonekano wanje na kama ujaanza kuchanua katika muonekano wanje jua ni mbegu iliyokaribia kuchepua ni wewe kutulia kuhakikisha mpaka inachipua.

Katika yeye kilindini kinaweza onekana nchi kavu, katika yeye ndani ya giza totoro unaweza ukaokota dhahabu inayoonekana peupe, na katika yeye unaweza kuvuka bahari kama unavuka barabara kwa miguu pasipo kuhofia chochote, katika yeye unaweza kukaa na mnyama mkali mathalani simba au chatu na bado ukaona usalama wako badala ya kuona ni hatari kwako wakawa ulinzi kwako.

Unaweza kukubali au kukataa! Unaweza kupenda au kutopenda! Unaweza kuchukia au kufurahi! Unaweza ng’ong’ona au kutoa sauti! Unaweza kuwaza au kutowaza! Hali yako au hali yoyote haiwezi badilisha hali hii kuwa yeye ANAITWA MUNGU. Na kwa lile analolikusudia kamwe uwezi kulizuia lisifanyike hata dunia yote ikiwa kinyume nae lakini yeye mwenyewe hawezi KUSHINDWA kutimiza hazima yake.

Hana ushemeji na mtu au ushikaji na mtu kwa kutegemea kwa wewe kufanya baadhi ya mambo unafikiri yapendazayo basi utapata kibali kwake Mungu! Kama hajafurahi basi hajafurahi tu unahitaji uelewe na kusimama katika njia upasayo kuenenda ili yeye afanye kama alivyokusudia na sio kufikiri utamshawishi Mungu kwakufanya baadhi ya mambo ayafurahiyo.

Hauhitaji kufika mbali sana na kupata picha zisizo kukusaidia katika maisha yako kama kuona hapa kuna ubaguzi, wenyewe, kujuana kwingi wewe tambua kuwa ANAITWA MUNGU mahali alipo ndipo kuna kunawiri na sio walipo watu wengi anapotengeneza njia hakuna awezae kuijua na hata kuizuia.

Usitafute mambo mengine yenye tija kwako na yasiyo na faida kwa Mungu mathalani kujulikana, kusifiwa kubali kutembea katika hatua za Mungu pasipo haraka kuliko kuwa na haraka pasipo kuona hatima njema katika maisha yako! KAMA YAKO NI YAKO TU MAANA ANAITWA MUNGU mtawala wa dunia na vyote vilivyopo ndani yake. Barikiwa rafiki!

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson………………………………………………0764 018535

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni