Jumanne, 2 Agosti 2016

USIIPENDE KESHO KAMA UJAIMALIZA LEO!



USIIPENDE KESHO KAMA UJAIMALIZA LEO


Hata paa likiwa linathamani kiasi gani lakini kamwe hauwezi  kulisimika kwanza alafu ukafuata msingi wa nyumba! KARIBU
 
Ni muhimu tuanze na MOJA na kisha twende kwenye MBILI, sio vizuri tu! ila pia inaleta maana! Ni vyema kuijenga vizuri msingi ili ikurahisishie kujenga nyumba imara na paa iweze kuwa na maana kuwepo maana dhuruba itakapo kuja haita iangusha maana usalama wa msingi utakuwa umeishikilia paa basi nawe utakaa salama na sio salama tu bali utayafurahia maisha yako! Karibu sana

Ni kawaida ya binadamu kupenda jambo jema na kuchukia jambo baya ni kawaida sana! Na katika muonekano wa jinsi hii utaitwa binadamu wa kawaida, kwa watu wenye akili zao watasema hasa huu ndio ubinadamu kuchukia lililobaya na kupenda kitu kizuri! 

Ni jambo jema sana kupenda kitu kizuri kwa kuwa kitu hicho kimekuwa kizuri kwa ajili ya kupendwa na sio kuchukiwa maana hilo silo lengo lake! Changamoto inakuja katika katika kukipata kitu kizuri maana kina vutia na wakati mwingine kinaweza kuwa na ushindani katika kukipata maana ni kitu kizuri hivyo kila mmoja anakihitaji japo inawezekana kwa lengo tofauti.

Sio kila jambo zuri utafikiria linafaa maadam umelifahamu kuwa ni jambo nzuri kila jambo zuri linakuwa la maana sana pindi utakapolitambua wakati wake sahihi! Niseme tu jambo sahihi linapofanywa katika hali sahihi basi kunakuwa na uwezesho uliobeba usahihi katika kukustawisha (mwenye akili njema).

Nikubaliane sana katika dunia ya sasa watu wamekuwa waki harakia mambo ya kesho kabla yakuimaliza leo wakiwa wanasababu nyingi mathalani nataka niwe wa kwanza mimi niitwe mvumbuzi au nisiwe boya, nikichelewa kitakuwa kimeisha, uwa mimi sipendi kujuta nataka niwai mapema ili nisijute!

Niseme kweli kuna mambo yanahitaji uwe na haraka ili kufanikisha mambo yaende sawa mathalani ajari lazima ufanyike uwezekano wa kuhakikisha usalama wa maisha yao waliojeruhiwa na mengine mengi lakini kamwe sio mambo yote au mengine yenye kivutio cha macho ya kakupa msukumo mkali pasipo kujua huu ni wakati wake wa mimi kuingia huku au kufanya hili.

*** Ni muhimu kujua kwamba kama ujaitendea haki leo basi jua hata kesho hautaitendea haki maana itakusumbua : usione watu wanakula basi nawe ukaingia kwenye kula lazima uangalia kweli wewe una njaa na ni kweli hicho chakula ni salama kwa kula! Na kweli ukila chakula hicho utashiba?

Ni muhimu kuwa na maswali yenye manufaa kwako ili kujiweka katika nafasi ya kutofanya makosa yasiyo ya lazima pindi utapoingia katika ulimwengu wowote mathalani URAFIKI, NDOA! Sio dhambi kuangalia katika ushirika huo mambo gani yanaendelea na majukumu gani yanaongezeka ila sio kwa kupa hofu bali katika kukupa kujipanga ili ufanye kitu kwa ubora pasipo KUMSINGIZIA SHETANI MAHALI AMBAPO YEYE AHUSIKI.

Alafu sio ujinga kuikamilisha LEO ikawa ni msingi wako mzuri wa kufanya KESHO kuwa yenye maana zaidi kwako, mathalani unaweza mtu anaweza kuwa mikakati mizuri ya biashara yake lakini baada ya kuona mwingine anauza zaidi kuliko yeye basi anafungua na yeye biashara kama ya yule jirani yake na baada ya muda yule akaacha ile biashara na yeye akaendelea hata baada ya mwingine kuacha pasipo kujua mwenzake ameacha kwa sababu msimu umeisha, au kunamtindo mpya umeingia unaanza kusema mimi nimerogwa au hapa sio bure alivyoondoka kaniachia uchawi ona sasa biashara inadoda.

Ishi maisha ya leo vizuri sana ili hata ikifika kesho usihitamani JANA, kwakua ulitendea ipasavyo na hivyo imekupa msingi mzuri wa wewe kufika hatua hiyo kwa ushindi.

Lazima uelewe kuwa Mungu aliiweka LEO na KESHO alikuwa na maana kubwa sana basi heshimu hilo na hakikisha huna haraka ya KESHO kama UJAIMALIZA LEO, kesho hipo tu hauhitaji kuikimbilia maana itakuja tu!

Imeandaliwa na:

Cothey  Nelson…………………………………………………….0764 018535

KESHO YAKO IKO MIKONONI MWA MUNGU! IKO SALAMA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni