Jumanne, 23 Agosti 2016

KINACHONIZUNGUKA KIMENITENGENEZA!



KINACHONIZUNGUKA KIMENITENGENEZA


Uwa atushangai sana kuona mmasai kuuza dawa za asili! Hama akivaa mashuka yake na kutembea barabarani hilo linakuwa ni swala la kawaida tu! Na pengine  japo mtu anaweza kutembea na rungu unaweza kumshangaa sana lakini pindi utakapo waona wamasai wengi wakitembea na rungu na huku wakicheka hauta shangaa sana kama ulivyo muona mtu asie mmasai ………….kwa nini? Na pindi unapomuona mmasai akila nyama ya ng’ombe uwezi kushangaa sana lakini pindi utakapo muona mmasai anakula samaki bila shaka hapo utaanza kuwa na maswali kichwani…………unafikiri ni kwa nini?

Tukiachana na wamasai maana hawa ni watu wazuri………..pindi unaweza kutoka na rafiki kwenda hotelini, aliyetokea kanda ya ziwa ukaona anaagiza samaki hasa aina sato bila shaka hauta shangaa…………hivi ni kwa nini? Ila unaweza kushangaa kidogo kuona muhaya pindi akiona senene anasikia kichefuchefu na kuhisi kutapika…..hivi ni kwa nini utashangaa!

Ukiwa mtafiti wa watu walifanikiwa/mashuhuri japo sio wote ila kwa asilimia kubwa utakuta familia zao zilikuwa namna yake mathalani wana muziki, wachoraji, wana michezo kwa ujumla wao ukiwafatilia vizuri kama sio tu juhudi zake binafsi basi ata mazingira yaliyo mzunguka yalipa nafasi nzuri katika kujifunza hicho kitu na hatimae akawa mahiri na kuwa kielelezo katika jamii yake na hata ulimwengu mzima.

Ndomana uwezi kushangaa watu waliotoka sehemu fulani kuwa wataalam katika jambo husika kwakua utakuta mtu amezaliwa na kukua katika mazingira hayo na hatimae akaona hayo kuwa ndio maisha yake mathalani uwezi kushangaa kuona watu wa kanda ya ziwa ni wazuri/mahiri katika uvuvi na upande wa muziki kuona watu wana uwezo mzuri kutoka baadhi ya maeneo uwa mahiri sana kuliko maeneo mengine mathalani unaweza usishangae ukisikia mtu toka MBEYA/KIGOMA anaimba lakini unaweza kuongeza umakini kidogo pindi ukiona MCHAGA anaimba sisemi watu hawa hawajui kuimba bali ni nadra kusikia.

Biblia inasema ushirika mbaya uharibu tabia njema! Kwa maana kile kinachokuzunguka na ulichokipa nafasi kina nafasi kubwa ya kukuathiri katika maisha yako na kukutengeneza kiasi kwamba mtu akikuona wewe atatambua CHIMBUKO LAKO! 

KARIBU!

Wako watu wamekuwa wakibadilika sana kutokana na mtu aliyekutana nae au hali fulani katika maisha yake inawezekana katika faida au hasara…….wako walikuwa watu wema sana ila baada ya kukutana na watu wengine wenye roho ya ukatiri ikamvika na hatimae ukatiri ukawa ni maisha yake na wako watu walikuwa wabaya na baada ya kukutana na watu wazuri wakawa watu wa maana sana wenye faida katika katika jamii,taifa na katika mataifa.

Hivyo ni muhimu kabla ujamhukumu mtu ni muhimu ni muhimu kutambua maamuzi yake ya leo yametengezwa na JANA yake ni muhimu kutambua jana ilikuaje na ndipo utafute namna ya kumsaidia katika ufasaha zaidi.

Ndomana mtu uliye muacha kwa kitambo kidogo na pindi unapokutana nae tena unaweza kukuta ana mabadiliko makubwa sana, inategemea amekutana na nani? Ambaye amemtengenezea muonekano mpya  ambao una uona sasa, usishangai kumkuta sasa pombe amekuwa rafiki yake, chumba chake kimekuwa fensi yake ya kutembea atoki tena kama zamani.

Unaweza kushangaa kuona mtu amekuwa na UPENDO, FURAHA NA KICHEKO ukaona mbona amekuwa tofauti na mwanzo hakuwa hivyo, jua kuna kitu amekutana nacho na hatimae kime mbadilisha

Nakubalina kwa asilimia kubwa ili mtu abadilike inategemea nani ameungamanisha nae na mala chache sana kuona mtu anabaidilika yeye mwenyewe tu labda NENO LA MUNGU na Mungu kwa namna yake!

Lakini kuna sababu zinazo wafanya watu wabadilike japo matawi ni mengi lakini kubwa ni moja tu ni USHIRIKA! Unaweza:

i.                    Urafiki

ii.                  Ndoa n.k

Unawa za kukuta mtu amebailika sana ni tofauti alivyokuwa kabla ya kuoa/ kuoelewa au ajakuwa na rafiki na mtu fulani ambaye akaingia katika maisha yake na kumtengeneza katika muonekano mwingine unaweza kuwa uliutegemea au usioutegemea.

Hivyo ni muhimu sana kuwa makini  katika muungamaniko ulionao unaweza kukutengeneza kuwa mbaya sana au kuwa mtu wa maana sana!

NIKUTAKIE KILA LA KHERI!
Imeandaliwa na:
Cothey  Nelson…………………………………………………………………0764 018535



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni