Jumanne, 30 Agosti 2016

DUNIA HAIWEZI KUKUPA PUMZIKO!



DUNIA HAIWEZI KUKUPA PUMZIKO


Moja ya vitu ambavyo DUNIA haiwezi kutoa ni PUMZIKO, japo watu wengi wanategemea sana na kungoja kuona DUNIA ikitoa PUMZIKO kwao, ili nao waweze kupata ahueni. Naweza kusema PUMZIKO ni rafiki wa kila mtu kwakua tuna amini kuwa katika pumziko basi hapo kuna raha, tulizo na amani kutokana na vitu hivyo basi watu upenda sana kuwa na PUMZIKO lakini wasiojue kuwa wapi ni sehemu sahihi ya kupata PUMZIKO.

Wako watu wanafikiri wakipata gari basi watapata pumziko lakini anaweza pata gari bado asilione pumziko na wakati mwingine akaona kero na gharama zimeongezeka, wengine wanasema wakisoma sana basi watapata pumziko na hatimae matarajio yao yatatimia lakini bado anakuwa anaona kama kitu alichofikiri atakipata hakipati, pia wako watu wengine wanafikiri wakijenga nyumba basi watapata pumziko lakini bado anajiona kama kuna kitu amekikosa na walio wengi inawezekana walifikiri au wanafikiri wakipa mchumba hapo atapata pumziko lakini ata baada ya kumpata na hata kufunga ndoa lakini mwisho anajiona bado ajapata kile anachokitaka.

Pumziko limekuwa ni swali lililokosa jibu! Kwani watu wengi wamejitahidi kwa uwezo wote kupata pumziko imekua kama zaidi ya tanzanite kutokana na uadimu wake mpaka imepelekea watu kuizoea hali iliyopo hata kama haipendi na kupoteza bidii yake ya kutafuta pumziko katika maisha yake kwakua anaona kutafuta pumziko imekuwa ni sawa na kutafuta chozi la samaki baharini.

Pumziko lingekuwa lina uzwa basi nafikiri hata masikini angejitahidi kwa hali na mali hata hauze mali zake ili mradi naye apate hilo PUMZIKO kwakua ana amini katika hilo anaweza pata usingizi wa furaha na amani, na hata akili yake kufanya kazi kiufasaha pasipo buguza yoyote, napengine ingeisha kutokana na wenye uwezo kuinunua na kuisha kabisa na wengine kukosa.

Lakini ashukuriwe Mungu PUMZIKO lipo ambalo hauhitaji uwe na kiasi cha fedha kikubwa ili uweze kununua kwani ni yeye mwenyewe anatoa, ila inakuwa ngumu sana kwakua yeye utoa kwa namna yake inje yake hakuna PUMZIKO lake.

Lakini dunia ya sasa tumekuwa tukitafuta sana pumziko katika njia isiyo sahihi uku tukimtupilimbali yeye mtoa pumziko ( Mungu), wako watu wamekuwa wakionga ili wapate pumziko, wakisema uongo ili wapate pumziko pasipo kujua pumziko alitokani na matamanio ya mwili bali ujazo waroho katika Mungu.

Pumziko imekuwa adimu sana katika dunia hii kutokana na kuitegemea dunia kwakua itatoa pumziko lakini imekuwa sivyo, imekuwa kama mtu anategemea kumuona mamba katika bahari na sio mtoni bila shaka unaweza kukesha hapo pasipo kuona dalili ya hata ya mkia wa mamba, japo unaweza kujifariji lakini sio kweli kila subira itavuta heri, ndo mana tumeona watu wakitumia njia zao zenye mwisho unaongeza msongo na mateso katika mwili mathalani mtu anakunywa pombe au kucheza mziki sana akitumai baada ya kucheza sana basi hata pata pumziko.

Na wengine wamekwenda mbali kidogo wakitumia muda mwingi wa kufikiria sana namna ya kutoka katika hali Fulani na hatimae kupata pumziko na kuleta furaha katika maisha yake lakini wakati mwingi imekuwa bado changamoto ikiisha hili linakuja hili unaweza kuitumia njia hiyo mwisho itakapo feli utashindwa kupata njia sahihi ya wewe kutoka hapo, usipo kuwa makini unaweza kusema kuwa hapa Mungu ayupo.

PUMZIKO!
Hili swala jepesi sana, kwanza niseme kwanza katika hali ya kawaida tu unafikiri pumziko la mtoto halisi atalipata wapi je! Kwa jirani  hama ndugu jamaa au rafiki wa wazazi ? na fikiri utakuwa umeshanielewa bila shaka mzazi ndie ajuaye tahamani ya mtoto na yeye ndie mwenye kuwajibika kuhakikisha kuwa mtoto anakuwa na furaha sana wakati wote na kama kile alichokuwa na uwezo nacho na anaona kuwa ni kitu chema kwa mtoto wake kamwe hawezi kumnyima,

Mathayo 7:11 Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa   vyema, je! Si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao?

Naamini umenielewa sana muache Mungu mwenyewe akupe PUMZIKO maana yeye anaijua KESHO KABLA YA LEO!

Niseme tu hakuna aliye tegemea pumziko kwa Mungu na Mungu asimpatie kama alivyosema basi atatekeleza, UKIMPATA MUNGU BASI UMEPATA PUMZIKO!

Imeandaliwa na:
Cothey  Nelson…………………………………………..……………………0764 018535
INAITWA SIKU! BARIKIWA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni