Jumanne, 16 Agosti 2016

SIJIONI!



SIJIONI



Wako watu wamekuwa waki wasumbua mafundi hasa wachereani kwakutaka mshono ambao utakuwa ni moja ya mtu fulani ambaye anampenda anavyo vaa pasipo kujua kwanini yule mtu alivaa vile? Ila wewe kwakua unampenda basi utamsumbua fundi utafikiri umemuajiri wewe ili mradi tu ufanane na mtu ambaye yeye mwenyewe hata ataki kukujua! Sio hao tu bali kuna watu wanaenda salon wakita minyoo/ kutengeneza nywele zinazofanana na watu waliokichwani mwao nao wanatumia muda mwingi kumuelekeza mwenye saloon kama yeye amelipia saloon siku nzima! 

Ni jambo ambalo mtu ulitegemea pindi anapojiangalia katika kioo ajione yeye maana hiyo ndio kazi moja wapo ya kioo kumuonyesha mtu jinsi anavyoonekana ili kumrahisishia katika kujirekebisha mahali penye upungufu ili kuwa bora zaidi au kughara zaidi au kuwa na muonekano ulio bora zaidi.
Sijui utajisikiaje pindi utakapoamua kujiangalia katika kioo ukawa UJIONI wewe ila unamuona mtu mwingine je! Utachukia au utaamua kubadilisha kioo ili kupata utofauti ili uone kama kuna mabadiliko yoyote! Au utajisikia sasa uko bomba!

Lakini katika dunia ya sasa watu wengi wamekuwa wakitamani pindi wakijiona wasiojione wao bali waone mfanano wa mtu mmoja mashuhuri katika ulimwengu! Na hata kuibuka mitindo mbalimbali ya nywele, nguo, muonekano na hata ongea ya mtu imebebwa na mtu mwingine! 

Siongelei wale wanaofanya vichekesho au maigizo bali nazungumzia mtu husika akiwa na akili timamu katika kukubali mtu mwingine aishi kupitia yeye azidi kumtambulisha mtu mmoja kwasababu yeye anampenda pasipo kujali wewe unamtambulisha je! Wewe nani atakutambulisha? Wako watu wanaita swaga………..!

Ukiangalia watu wanamna hii unaweza kusema wanaweza kumuuliza Mungu kwanini umeniumba hivi ukiniumba vile hama kwanini mimi sikuzaliwa marekani ni kazaliwa bara la giza! Ukimuangalia jinsi mtu anavyojiangalia namna anavyoenda ni vitu fulani hivi ambavyo haviendani kabisa,

Kweli katika ulimwengu wa sasa watu wengi wamepoteza utambulisho wao,utaweza kuona mtu sio kwamba anatamani kufanikiwa kama mtu mashuhuri alivyo fanikiwa bali uanza kuishi kivuli cha mtu katika muonekano usiofanana bali unaolazimishwa kufanana mathalani mtu anampenda mchezaji messi basi utakuta mtu anataka kuvaa kaptura kama anayo vaa messi pasipo kujua yeye anavaa vile kwa sababu ya nini sio hilo tu hadi kutembea, kushangilia ili mradi yeye aonekane kuwa yeye ana mapenzi ya dhati na mchezaji huyo.

Sio mfanano katika hilo bali hali uoenekana katika fani mbalimbali muziki, mitindo na hata filamu mtu utaka kuenenda katika muonekano wa mtu fulani, pasipo kujua kwa kiasi kikubwa katika kufanya hivyo unapoteza utambulisho wako ambao Mungu ameweka  ndani yako ili kuleta msaada kwa jamii fulani ambayo Mungu amekupa neema ya wewe kuwepo.

Maisha haya upelekea kutoishi wewe bali yeye kuishi kupitia wewe inakuwa kama wewe ukupaswa kuwepo kwakua pacha wako ameshatokea kwakua yote anayo  yafanya yeye ndiyo wewe unayafanya baada ya kuona yeye anafanya, bila shaka unakandamiza ile hazina ambayo Mungu ameiweka ndani yako kwa kua unaiona haina thamani ila ya wengine ndio iliyo bora kwakua imeshatambulika na kupata kibali mioyoni mwa watu! Pasipo jua kuwa hata wewe ukiamua kukipenda kilicho chako watu wengine watakipenda tu na hata wasipo kipenda wewe unamalizana na Mungu kwa kutumia kile ulichopewa na Mungu.

Kupenda au kumkubali mtu katika kitu kizuri anachokifanya sio vibaya ila sio vyema kupoteza au kutotumia hazina ambayo Mungu ameweka ndani yako! Maana utakuta mtu anavyompenda mtu hadi unashanga……..utakuata anataka apige mswaki kama yule, acheke kama yule, alale kama yule na hata kulia kama yule basi hapakuwa sababu ya wewe kuwepo, tambua Mungu kumuumba yule na WEWE  kuna sababu na wala haikuwa kwa bahati.

Kupenda kitu kizuri anachokifanya mwingine ni vizuri kwani Mungu amesema TUPENDANE ni sawa na ni vizuri lakini sio watu wakikuona wewe wamuone mtu mwingine kabisa ambaye anaushirikiano na wewe kabisa.

Ni vizuri kujifunza mambo mazuri kwakua ni jambo jema litakuongeza katika lile ambalo unalolifanya ili liwe bora zaidi zaidi, kwani kila utendaji wa mtu una mapungufu yake hivyo utakapo kuwa pale utajifunza vyema ili usifanye makosa tena bali uendelee mbele katika ubora mpya.

Imeandaliwa na:

Cothey Nelson……………………………………………………………0764 018535

JITHAMINI UTATHAMINIKA-------JIONE MWENYEWE MAANA WEWE NI BORA!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni